Ritifaa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Apostrofi)
Apostrofi au ritifaa.

Ritifaa (kutoka neno la Kiarabu; pia apostrofi kutoka Kigiriki ἀποστροφή, apostrofee, "ondoleo", kupitia Kiingereza: "apostrophe"; huitwa tena king'ong'o) ni alama ya uakifishaji inayoandikwa '.

Umbo lake ni sawa na mkato lakini inakaa juu ya mstari.

Alama hiyo inaonyesha pengine kwamba herufi au silabi imeanguka au kupunguzwa, kwa mfano katika shairi, lakini katika herufi "ng'" inatofautisha fonimu husika na nyingine inayofanana (ng). Baadhi ya maneno yenye apostrofi ni ng'ombe na kung'ata.

Kwa Kiingereza ni alama inayotumika zaidi kuonyesha hali ya jambo kuwa mali ya fulani: * Mike's car = gari la Mike.

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ritifaa kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.