Alex Song

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jina kamili la Alex Song ni Alexandre Dimitri Song Billong
{{{jinalamchezaji}}}
Maelezo binafsi
Tarehe ya kuzaliwa {{{tareheyakuzaliwa}}}
Mahala pa kuzaliwa    {{{nchialiozaliwa}}}

* Magoli alioshinda

Alexandre Dimitri Song Billong (mara nyingi hujulikana kama Alex Song; alizaliwa mnamo 9 Septemba 1987) ni mwanakandanda wa kulipwa kutoka nchi ya Kamerun ambaye anaichezea klabu ya Arsenal Ligi Kuu ya Uingereza.

Yeye ni mpwa wa Rigobert Song na hucheza kama kiungo wa kati anayelinda safu ya ulinzi ya difenda wanne na pia amecheza kama difenda wa kati katika safu ya ulinzi. Awali hakuwa anaichezea timu ya kwanza lakini kwa haraka akawa sehemu muhimu ya timu ya kwanza wakati wa msimu wa 2008-09 na alianza mechi nyingi.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Song alizaliwa katika mji mkuu wa Douala nchini Kamerun na kupoteza baba yake akiwa na umri wa miaka tatu. Tangu wakati huo, mjomba wake maarufu zaidi, Rigobert Song, amekuwa kama babake wa pili na alikuwa mshawishi mkubwa katika kumfanya Alex kuchagua kandanda kama wasifu. Alex Song alitaka kuwapa watoto wake malezi mazuri katika maisha, ambayo anadai hakuipata yeye; alioa akiwa na umri wa miaka 18 na sasa ni baba wa watoto wawili, na yule mkubwa ana umri wa miaka miwili na anaitwa Nolan.

Wasifu wa Klabu[hariri | hariri chanzo]

Bastia[hariri | hariri chanzo]

Song alijiunga na timu ya vijana ya Bastia katika msimu wa 2003-04 na sehemu muhimu ya timu ya kwanza msimu uliyofuata kwani alicheza mechi 34. Katika wakati wake akiichezea klabu ya Bastia, alivutia usikivu kutoka idadi ya klabu mbalimbali zikiwa ni pamoja na Inter Milan, Manchester United, Lyon, na Middlesbrough. Hata hivyo, alimvutia na kumsisimua sana meneja wa Arsenal, Arsène Wenger, kama mchezaji aliyekuwa majaribioni katika kambi ya mazoezi ya kabla ya kufungua msimu nchini Austria, na Arsenal walipata huduma zake kwa mkopo kwa ajili ya msimu wa 2005-06. Arsenal ilikubali kumnunua kwa kitita cha paundi (£) milioni 1 [6] mwezi Juni mwaka wa 2006 na alisaini mkataba wa miaka minne.

Arsenal[hariri | hariri chanzo]

Song alicheza mechi yake ya kwanza ya ligi kuu ya Uingereza katika ushindi wa Arsenal wa 2-0 dhidi ya Everton mnamo 19 Septemba 2005 kama mbadala. Alicheza mechi kadhaa za ligi ya mabingwa barani Ulaya na alianza mechi kadhaa za ligi kuu ya Uingereza msimu huo ukikaribia kwisha, wakati wachezaji wa timu ya kwanza walikuwa wamejeruhiwa au walikuwa wamepumzishwa.

Alifunga bao lake la kwanza la Arsenal dhidi ya Liverpool katika ushindi wa Arsenal wa 6-3 win katika uwanja wa Anfield katika Kombe la Carling mnamo 9 Januari 2007.

Mnamo 30 Januari 2007, ilithibitisha kuwa Charlton Athletic ilikuwa imemsaini Song kwa mkopo hadi mwisho wa msimu wa 2006-07. Ingawa alisisimua, Charlton ilishukishwa ngazi hadi daraja wa pili na Song alirudi kuichezea Arsenal.

Katika msimu wa 2007-08, Song alianza kama difenda wa kati katika safu ya ulinzi ya katika mechi za Arsenal za kombe la Carling, lakini alikosa nusu fainali yao ambapo walibanduliwa nje kombe hilo na Tottenham wakati alikuwa ameenda kuichezea Kamerun katika Kombe la Mataifa ya Afrika. Pia alianza kama difenda wa kati katika safu ya ulinzu katika mechi za mwisho msimu huo ukienda kutamtishwa, hasa katika ziara muhimu ya Arsenal katika uwanja wa OLD TRAFFORD dhidi ya Manchester United, huku difenda wa kati Kolo Toure akianzishwa upande wa kulia wa safu ya ulinzi katika nafasu ya Bacary Sagna.

Alifunga bao katika ushindi wa Arsenal wa 5-2 ugenini dhidi ya Fenerbahce katika shindano la kombe la mabingwa barani Ulaya. Bao la kwanza la Song katika ligi kuu ya Uingereza, na la tatu katika mashindano yote ya Gunners, lilifungwa dhidi ya Wigan Athletic mnamo 11 Aprili 2009 ambapo alipambana na wachezaji kadhaa na kisha kumaliza vizuri katika kona ya chini. Arsenal ilishinda mechi hiyo 4-1. Alikosolewa awali na baadhi ya makritiki kwa sababu ya kukosa uzoefu lakini baadaye alipata sifa kwa kuwa mmoja wa watendaji thabiti zaidi katika kampeni ambayo Arsenal ilimaliza bila nyara.

Msimu wa 2009/10[hariri | hariri chanzo]

Song alianza msimu vyema, kwa kucheza mechi 11 kwa 12 za ligi kuu ya Uingereza. Aliteuliwa katika nafasi ya tatu katika tuzo la Arsenal.com la mchezaji wa mwezi wa Oktoba, nyuma ya mshindi Cesc Fabregas na mchezaji aliyekuwa katika nafasi ya pili, Robin van Persie. Baada ya kuonyesha mchezo wa kusisimua katika moyo wa kiungo cha kati na kuwaruhusu washambuliaji bunifu wa Arsenal kuendesha kazi kwa ufanisi, Alex Song kwa sasa ni mmojawapo wa jina za kwanza katika orodha ya timu ya kwanza.

Kama ilivyothibitishwa mnamo Jumanne 25 Novemba 2009 katika mkutano wa Arsène Wenger wa baada mechi, Alex Song alisaini mkataba mpya wa muda mrefu na Arsenal, ambayo itadumu hadi mwaka wa 2014.

Mnamo 30 Desemba 2009, Song alifunga bao lake la pili katika ligi kuu ya Uingereza kwa Arsenal wakati alifunga bao la mwisho katika ushindi wa 4-1 dhidi ya Portsmouth.

Wasifu wa Kimataifa[hariri | hariri chanzo]

Ingawa hakuwa ameichezea timu ya kitaifa ya Kamerun wakati huo, Song alitajwa katika kikosi kwa Kamerun kwa ajili ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya mwaka wa 2008. Alicheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa ya Cameroon katika mechi yao ya kwanza ya kundi, ambayo walishindwa 4-2 dhidi ya wamiliki wa kombe hilo, Misri; aliingia kama mbadala wa Stephane Mbia baada ya nusu ya kwanza na alijiunga na mjomba wake Rigobert kwenye uwanja. Kwa muda wa michuano hiyo alikuwa ufunuo katika safu ya ulinzi ya Kamerun, na alipewa tuzo la mchezaji bora wa mechi katika nusu fainali ya Kamerun, lakini aliondolewa kwenye fainali dhidi ya Misri baada ya kujeruhiwa. Hata hivyo alitajwa katika timu ya mchuano ya wachezaji 11, sambamba na kiungo wa kati wa Newcastle na mwenzake wa Kamerun Geremi.

Takwimu ya Wasifu wa Arsenal[hariri | hariri chanzo]

(sahihi tangu 5 Desemba 2009)
Klabu Msimu Ligi! Kombe! Ulaya Jumla
Matokeo Mabao Usaidizi Matokeo Mabao Usaidizi Matokeo Mabao Usaidizi Matokeo Mabao Usaidizi
Arsenal 2005-06 5 0 0 2 0 0 2 0 0 9 0 0
2006-07 2 0 0 3 [1] 0 [1] 0 0 6. [1] 0
2007-08 9 0 0 3 0 0 3 0 0 15 0 [1]
2008-09 31 [1] [1] 6. 0 2 11 [1] 0 48 2 3
2009-10 17 [1] [1] 2 0 0 8 0 [1] 26 [1] 2
Jumla [61] 2 [1] 16 [1] 2 25 [1] [1] 104 4 6.

(* Kombe la FA, Kombe la Carling na FA Community Shield)

Tuzo[hariri | hariri chanzo]

Kamerun Nafasi ya pili

Binafsi

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: