Abedi Amani Karume
Mandhari
(Elekezwa kutoka Abeid Karume)

Sheikh Abeid Amani Karume (4 Agosti 1905 - 7 Aprili 1972) alikuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar. Aliongoza nchi hiyo mara baada ya mapinduzi yaliyomwangusha Sultani aliyekuwa akitawala Zanzibar hadi mwanzoni mwa mwaka 1964.
Baada ya miezi mitatu Zanzibar iliungana na Tanganyika iliyokuwa ikiongozwa na Mwalimu Nyerere. Baada ya muungano wa nchi hizo mbili uliozaa Tanzania, Karume alikuwa makamu wa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aliuawa kwa kupigwa risasi.
Kwa heshima yake, kila mwaka tarehe aliyofariki duniani ni sikukuu ya taifa kote nchini Tanzania.
Mtoto wake, Amani Abeid Karume, alikuwa rais wa Zanzibar tangu mwaka 2000 hadi 2010.
| Alitanguliwa na Nafasi ilivyoundwa |
Makamu wa Rais wa Tanzania 1964-1972 |
Akafuatiwa na Mwinyi Aboud Jumbe |