Umeme wa upepo
Umeme wa upepo ni umeme unaopatikana kwa njia ya mitambo inayotumia nguvu ya upepo na kuibadilisha kuwa umeme. [1]
Mwisho wa mwaka 2009 takriban asilimia 1.3 ya mahitaji ya umeme duniani zilikuwa umeme wa upepo. [2] Lakini nchi kadhaa zilizotangulia kuendesha teknolojia hii zinapata kiasi kikubwa zaidi. Nchi inayopata kiwango kikubwa cha mahitaji yake ya umeme ni Denmark yenye asilimia 20 za umeme wa upepo. [3][4] Katika Hispania ni 11% na 9% katika Eire. [5]
Katika Afrika ni hasa Afrika Kusini iliyoanza kutumia chanzo hiki cha nishati. Nchini Kenya Mradi wa umeme wa upepo wa Ziwa Turkana ulianzishwa mwaka 2010 unaotegea kutoa megawati 300 baada ya kukamilika.[6]
Jinsi ya kutumia nguvu ya upepo [hariri]
Upepo hutumiwa kuzungusha rafadha au parapela. Mwendo wa rafadha inaendelea kuzungusha jenereta ya kutoa umeme.
Marejeo ya Nje [hariri]
- ↑ Wind power in the UK. BBC News (2007-12-18). Rudishwa juu ya 2010-03-10.
- ↑ World Wind Energy Association (2008). Wind turbines generate more than 1 % of the global electricity
- ↑ Global wind energy markets continue to boom – 2006 another record year (PDF).
- ↑ Global Wind Energy Council (2009). Global Wind 2008 Report, p. 9, accessed on 4 Januari 2010.
- ↑ International Energy Agency (2009). IEA Wind Energy: Annual Report 2008 p. 9.
- ↑ http://laketurkanawindpower.com/