Servulo wa Roma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Servulo wa Roma (alifariki Roma, Italia, 23 Desemba 590) alikuwa ombaomba jijini Roma tangu utotoni kutokana na hali yake ya kupooza mwili mzima[1].

Pamoja na mateso yake hayo, aliishi kwa imani kubwa na kuwagawia maskini wenzake alichopewa na wafadhili.

Papa Gregori I aliandika juu yake sura moja ya kitabu cha Majadiliano.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 23 Desemba[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.