Marco Polo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mchoro wa sura ya Marco Polo.

Marco Polo (15 Septemba 12548 Januari 1324) alikuwa mpelelezi na mfanyabiashara wa Kiitalia. Ndiye wa kwanza kufanya upelelezi katika nchi zilizokingama na bara la Asia na “Mashariki ya Mbali” na wa kwanza kufanya upelelezi duniani kwa jumla.

Alichangamsha Ulaya nzima kwa kusimulia habari za safari zake katika kitabu "Il Milione" (yaani Milioni)

Inasemekana kuwa Marco Polo, ndiye aliyeleta chakula cha spaghetti nchini Italia. Alikipata chakula hicho huko Uchina na kukipeleka kwao.

Kati ya wapelelezi wengine wa Italia alikuwepo Christopher Columbus, ambaye alifuata nyayo za Marco, lakini kupitia magharibi.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mwandishi fulani wa Ulaya bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Marco Polo kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.