Johannes Kepler
Johannes Kepler (27 Desemba 1571 – 15 Novemba 1630) alikuwa mtaalamu wa astronomia, hisabati, teolojia na muziki kutoka nchini Ujerumani. Amekuwa maarafu hasa kwa sababu alitambua kanuni za mwendo wa sayari zikizunguka jua.
Kazi yake[hariri]
Alianza kazi yake kama mwalimu wa hisabati kwenye chuo cha Kiprotestanti mjini Graz (Austria). Baadaye aliitiwa Praha (leo nchini Ucheki) kama msaidizi wa Tycho Brahe aliyekuwa mwanahisabati rasmi wa Kaisari Rudolph II. Baadaye Kepler alipewa wajibu huu.
Kepler alitambua ya kwamba makadirio ya Nikolaus Kopernikus yalionyesha hali halisi, maana yake sayari pamoja na dunia zinazunguka jua. Hadi wakati ule wataalamu waliamini ya kwamba dunia yetu iko katikati ya ulimwengu na jua pamoja na sayari zinazunguka dunia.
Kanuni za mwendo wa sayari[hariri]
- Kanuni ya kwanza inasema sayari inatembea njia yenye umbo la duaradufu, si duara kamili, ikizungukia jua. Kabla ya Kepler wanaastronomia waliona njia ya sayari ni duara kamili.
- Kanuni ya pili inasema ya kwamba sayari inaongeza mwendo ikikaribia jua, lakini inapunguza mwendo ikienda mbali na jua.
- Kanuni ya tatu inaeleza ya kwamba sayari iliyo karibu na jua ina mkasi mkubwa kuliko sayari ambayo ni mbali.
Kwa kanuni zake aliweza kutabiri mahali pa sayari angani vizuri kushinda wataalamu wote waliomtangulia.
Viungo vya Nje[hariri]
- Annotation: Posner Family Collection in Electronic Format Harmonices mundi ("The Harmony of the Worlds") in fulltext facsimile; Kilatini
- Electronic facsimile-editions of the rare book collection at the Vienna Institute of Astronomy
- Kepler and the "Music of the Spheres"
- Gale E. Christianson- Kepler's Somnium: Science Fiction and the Renaissance Scientist
- Kepler's Belief in Astrology by Nick Kollerstrom
- References for Johannes Kepler