Benjamin wa Mambo Jambo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Benjamin wa Mambo Jambo
Kutoka kushoto ni: G Stable, Only Face na mwisho kabisa ni Benjamin mwenyewe.
Kutoka kushoto ni: G Stable, Only Face na mwisho kabisa ni Benjamin mwenyewe.
Maelezo ya awali
Jina la kuzaliwa Benjamin Sixtus Busungu
Pia anajulikana kama Benjamin
Amezaliwa 11 Novemba 1976 (1976-11-11) (umri 47)
Asili yake Sengerema, Mwanza
Tanzania
Aina ya muziki Hip hop
Afro-Pop
Dancehall
Bongo Flava
Kazi yake Singer/Producer
Ala Sauti
Miaka ya kazi 2000 - hadi leo
Studio Mwamba Productions
Mzuka Records
FM Studio
Kokwa Production
Napol Music
Ame/Wameshirikiana na Dknob
Saida Karoli
Zola D
Sharama
Papii Kocha
Baba Nyau
MC Chichi Bella
Tovuti https://web.facebook.com/benjaminwamambojambo/

https://www.instagram.com/benjaminwamambojambo/ https://open.spotify.com/artist/2xoxvoZEXPiijYGCGi2jgr

Benjamin Sixtus Busungu (anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Benjamin wa Mambo Jambo; alizaliwa tarehe 11 Novemba 1976) ni msanii mwimbaji wa Hip Hop, Dancehall, Afro-Beat, Afro-Pop na pia mtayarishaji wa rekodi kutoka nchini Tanzania.

Awali alikuwa na kundi la Mambo Jambo, kundi ambao lilikuwa linafanya muziki wa hip hop katika miaka ya 2001/2002.

Vibao vyake binafsi ni pamoja na: "Nimefulia", "Myfriend" na "Bang"[1] na "Mdundiko", na kuweza kushirikishwa katika baadhi ya nyimbo za bongo flava na albamu kadhaa. Vilevile amepiga video za muziki mbalimbali nchini Tanzania.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Benjamin alizaliwa katika hospitali ya Bombo mjini Tanga, Tanzania.

Ni mtoto wa nne kuzaliwa katika orodha ya watoto kumi wa Sixtus Busungu. Alianza elimu yake ya msingi kunako mwaka wa 1985 hadi 1991, katika shule ya msingi Mtejeta, wilaya ya Mpwapwa, katika mkoa wa Dodoma, Tanzania.

Kisha akaenda kujiunga na shule ya Sekondari ya Lake ya mjini Mwanza Tanzania, kwa kidato cha kwanza hadi cha nne akiwa hukohuko Mwanza.

Baada ya hapo, akaelekea zake katika mafunzo ya sanaa katika Chuo cha Sanaa cha Bagamoyo kuanzia 1998 hadi 2000.

Kwa sasa anasomea bachela ya utayarishaji wa filamu katika chuo cha AFDA kilichopo Cape Town, Afrika Kusini.

Mengine aliyosomea ni ufundi wa kompyuta na uhandisi wa sauti katika Dar Computer UDSM.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Bang ya Benjamini Mkono mpya wa Benja na Miikka Mwamba

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mwanamuziki/wanamuziki fulani wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Benjamin wa Mambo Jambo kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.