Albert Einstein
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Albert Einstein (14 Machi, 1879 – 18 Aprili, 1955) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ujerumani. Baadaye alihamia Marekani. Hasa anajulikana kwa nadharia yake inayolingana nishati na tungamo katika fomyula E = mc2. Mwaka wa 1921 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.

