Zoeradi na Benedikto

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Watakatifu Zoeradi na Benedikto.

Zoeradi na Benedikto (karne ya 10 - karne ya 11) walikuwa wakaapweke huko Nitra, leo nchini Slovakia.

Zoeradi (kutoka Opatowiec, Kazimierza, Polandi, mwaka 980 hivi) alipata kuwa mmonaki Mbenedikto kwa jina la Andrea nchini Hungaria, halafu alikubaliwa na abati wa monasteri yake kwenda kuishi upwekeni kama alivyofanya kwanza kwao.

Huko, alipata mfuasi mwenyeji, jina lake Benedikto wa Skalka, akashika pamoja naye maisha magumu sana[1][2].

Papa Gregori VII mwaka 1083 aliwatangaza pamoja kuwa watakatifu.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 17 Julai[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://books.google.com/books?id=4CTabJd9p7YC&dq=Benedict+of+Szkalka&pg=PA55 Mackenzie, Georgina Muir and Irby, Adelina Paulina. Across the Carpathians, Macmillan, 1862, p. 54
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/63170
  3. Martyrologium Romanum

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Hoffmann H.: Die Heilige Zoerad. Archiv für schlesische Kirchengeschichte 3. 1938, p. 283-286.
  • Semkowicz Władysław: Andrzej Świerad. In: Polski Słownik Biograficzny. Vol. 1. 1935, p. 100-101.
  • Silnicki T.: Dzieje Kościoła na Śląsku. Warszawa 1953, p. 25, 94.
  • Wędzki Andrzej: Andrzej-Świerad. In: Słownik Starożytności Słowiańskich. Vol. 1961, p. 24-25.
  • Wojciechowski Tadeusz: Eremici reguły św. Romualda. In: Szkice historyczne XI wieku. Kraków 1904, p. 53-58.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.