Yericko Y. Nyerere
Yericko Nyerere | |
![]() | |
Amezaliwa | 14 Aprili 1983 Iringa, Tanzania |
---|---|
Nchi | Tanzania |
Kazi yake | Muandishi wa vitabu |
Chama cha kisiasa | CHADEMA |
Yericko Yohanesy Msambila Mkana Nyerere (alizaliwa katika Kijiji cha Maduma, wilaya ya Mufindi, mkoa wa Iringa, Tanzania, 4 Aprili 1983), ni mfanyabiashara mwanzilishi wa kampuni ya "Yecco Group Limited". Ni mwanachama na mjumbe wa Mkutano Mkuu wa chama cha kisiasa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Yericko Yohanesy Nyerere ni mshindi wa tuzo 6 mfululizo "Barani Afrika", ambapo tuzo 5 ni za "Mwandishi Bora wa Vitabu Afrika", na tuzo 1 ni ya "Kiongozi Bora wa Kijamii Afrika",
Yericko ameshinda tuzo ya Mwandishi Bora wa Vitabu iliyotolewa na “Young Achievement Africa Awards 2025”, Kisha akashinda tuzo "Shining Stars Africa Awards 2024”.
Mwaka huohuo 2024 alishinda tuzo ya "Music Video Africa Awards" (MVAA) akishinda mara moja.
Na mwaka 2024 Yericko alishinda tuzo za "Zikomo Africa Awards". Lakini pia tuzo hiyohiyo ya Zikomo alishinda mwaka 2023.
Tuzo za uandishi wa vitabu alishinda kupitia Vitabu vyake kama vile kitabu cha "Ujasusi wa Kidola na Kichumi", toleo la 2016, Kitabu cha "Mapambano ya Madaraka", toleo la 2017, kitabu cha "Mtu Baada ya Mtu", toleo la 2020 na Kitabu cha “We Shall Win” toleo la 2025.
[1] Yericko pia mtanzania wa pili kutangaza hadharani kuwa anaabudu dini za Kiafrika za asili (Mizimu), akiungana na Mtanzania mwingine Hayati Kingunge Ngombare Mwilu ambae nae aliabudu Mizimu. Hivyo yeye si "Mkristo" wala "Muislamu".
Urithi wake wa fasihi juu ya uandishi pia unadhihirishwa juu ya mkakati wa ushindi wa ushirika wa vyama wa vyama pinzani nchini Tanzania (UKAWA) wakati wa uchaguzi mkuu mwaka 2015 akiwa sehemu ya jopo la wanamikakati wa Chama.
Elimu
[hariri | hariri chanzo]Yericko ana Stashahada ya Saikolojia ya kiuchunguzi kutoka katika chuo kikuu huria cha Uingereza (2016-2017), akapata Stashahada ya Uchunguzi na Upelelezi kutoka taasisi ya kimataifa ya Uchunguzi na upelelezi ya "International Institute Of Certified Forensic Investigation Professionals" kwa kushirikiana na "Osulivan Associates International" - USA (2015).
Kazi
[hariri | hariri chanzo]Tangu 2010 hadi Julai 2015, Yericko Nyerere alikuwa mshauri wa Usalama na Ulinzi binafsi kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Willibrod Peter Slaa. Kama mwanaharakati wa kisiasa anasifika kwa mazungumzo yake ya busara juu ya mabadiliko ya kisiasa na maendeleo ya kiuchumi nchini Tanzania, kazi zake hasa vitabu na makala mitandaoni zimesababisha ushawishi mkubwa kwa kura nyingi kwa watoa maamuzi na viongozi wa kisiasa. Amekuwa msukumo wa kisiasa kwa mabadiliko na ushiriki wa vijana na ushiriki katika ajenda ya serikali na mabadiliko ya kiuchumi.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "UU Ventures". www.uu.com. Iliwekwa mnamo 2024-12-18.
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- https://mtanzania.co.tz/yeriko-nyerere-kizimbani-kwa-uchochezi-facebook/
- https://www.dw.com/sw/yericko-nyerere-azungumzia-orodha-ya-watu-hatari/av-42753403
- https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/yericko-nyerere-alipa-faini-akwepa-kifungo-miaka-mitatu-jela-3333184%3fview=htmlamp Ilihifadhiwa 24 Machi 2021 kwenye Wayback Machine.
- https://www.rfi.fr/sw/makala/afrika-ya-mashariki/20210727-utamaduni-wa-kuandika-na-kusoma-vitabu-nchini-tanzania
- https://searchworks.stanford.edu/view/12863187
- https://www.amazon.com/s?k=Yericko+Nyerere
- https://iicfip.org/tanzania-2/
- https://www.futurelearn.com/certificates/8033r09
- https://crb.go.tz/contractordetails/home/search?search=Yecco Ilihifadhiwa 6 Septemba 2021 kwenye Wayback Machine.
- https://catalog.loc.gov/vwebv/search?searchArg=Yericko+Nyerere&searchCode=GKEY%5E*&searchType=0&recCount=25
- https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/yeriko-nyerere-afikishwa-mahakamani--2793292?view=htmlamp
![]() |
Makala hii kuhusu mwandishi fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Yericko Y. Nyerere kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |