Wuhan

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Jiji la Wuhan
Jiji la Wuhan is located in China
Jiji la Wuhan
Jiji la Wuhan

Mahali pa Wuhan katika China

Majiranukta: 29°58′20″N 113°53′29″E / 29.97222°N 113.89139°E / 29.97222; 113.89139
Nchi China
Jimbo Hubei
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 9,760,000 (2,007)
Tovuti:  http://www.wuhan.gov.cn/
Wuhan
Mahali pa Wuhan katika mkoa wa Hubei

Wuhan (kwa Kichina: 武汉) ni mji wa China. Ndio mji mkuu wa jimbo la Hubei.

Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa 2007, kuna wakazi wapatao milioni 9.8 wanaoishi katika mji huu[1]. Hivyo si mji mkubwa zaidi katika Hubei pekee, bali ni jiji kubwa zaidi katika China ya Kati.

Ni mji wenye tasnia nyingi, kuanzia makampuni yanayozalisha motokaa hadi makampuni ya teknolojia mpya kama kompyuta, pamoja na taasisi za utafiti wa kisayansi zaidi ya 300 [2].

Mwaka 2020 jina la Wuhan lilitajwa kote duniani kutokana na uenezi wa virusi hatari vya corona ambao ulisababisha vifo vya watu zaidi ya elfu moja pamoja na hofu ya epidemiki[3]. Jiji lote liliwekwa na serikali kuu katika hali ya karantini. Kabla ya tangazo hilo watu milioni 5 waliondoka mjini[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. OECD Urban Policy Reviews: China 2015, tovuti ya OECD library, iliangaliwa Januari 2020
  2. Focus on Wuhan, China, tovuti ya Canadian Trade Commissioner Service, 2007
  3. China's unprecedented reaction to the Wuhan virus probably couldn't be pulled off in any other country, tovuti ya CNN tar. 27-01-2020
  4. 5 million people left Wuhan before China quarantined the city to contain the coronavirus outbreak, taarifa ya gazeti Business Insider USA, kupitia www.pulselive.co.ke, tarehe 27-01-2020
Makala hii kuhusu maeneo ya China bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Wuhan kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.