Nenda kwa yaliyomo

Vicensia Fuko

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Vicensia Alfred Fuko
Amezaliwa
Tanzania
Nchi Bendera ya Tanzania Tanzania
Majina mengine Geline Alfred Fuko
Kazi yake Mwanasheria

Vicensia Alfred Fuko ni Mtanzania mwanasheria, mwanaharakati wa haki za binadamu na mtaalamu katika usimamizi na uratibu wa programu mbalimbali za uandishi wa habari, sheria za vyombo vya habari, vikiwa pamoja na vyombo vya habari vya kidigiti, ambaye ni mhitimu wa Shahada ya uzamivu kupitia programu ya Erasmus Mundus Joint katika Maendeleo ya jamii.[1][2]

Amesaidia kukuza demokrasia nchini Tanzania katika mashirika kama Tangible Initiatives For Local Development Tanzania (TIFLD) ambapo alikuwa na mchango mkubwa katika kubuni na kusimamia mfumo wa kwanza wa mtandao wa kuhifadhi data ya umma kwenye rasilimali za kikatiba.[3][4] Mafanikio yake yalitambuliwa wazi na Rais Obama katika Mkutano wa Rais wa YALI huko Washington, D.C. mnamo 3 Agosti 2016.[5]

Kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, aliteuliwa kuwa meneja wa TACCEO Election Observation Center akiwa chini ya mwavuli wa asasi za kiraia 16.[6]

Masomo yake ya shule ya msingi mpaka sekondari aliyapata katika mikoa ya Ruvuma, Singida na Tanga kabla ya kujiunga na shule ya sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuhitimu mnamo 2007. Mnamo mwaka 2010, alirejea masomoni kupitia programu ya Erasmus Mundus master's degree,[7] akitumia miezi tisa nchini Italia, na vipindi vifupi katika Chuo Kikuu cha Corvinus huko Budapest, Hungaria, na kikundi cha wanaojitolea cha Umoja wa Mataifa huko Bonn nchini Ujerumani. Kisha akarudi Italia ambapo alihitimu shahidi ya uzamivu utoka Chuo Kikuu cha Trento mnamo 2012.[8]

Hivyo Vicensia ana shahada ya pili ya sheria katika sheria (LL.M.) ya Mali ya Kimaadili kutoka Chuo Kikuu cha Stockholm na shahada ya kwanza ya sheria (LL.B.) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mwaka wa 2017 alichaguliwa kuwa mshirika wa Mandela Washington kuwekwa Chuo Kikuu cha Delaware huko Newark. Baada ya kumaliza mafunzo katika Chuo Kikuu cha Delaware, Vicensia alikuwa na mipango ya kuendelea kusimamia maabara na ushirika na miradi ya ushirikiano wa kimkakati ili kukuza uhuru wa kujieleza, upatikanaji wa habari, na uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania. [9][10]

Kama wahitimu uwanasheria na kutokana na kupendezwa kwake na haki za binadamu, Fuko kwanza alifanya kazi kwa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali ya haki za binadamu ambapo alifuatilia vikao vya bunge na sheria zinazoibuka, na kutoa huduma ya habari kwa umma.[8]

Aliporudi kutoka masomo yake ya Erasmus, alifanya kazi na mashirika anuwai ya haki za binadamu ikijumuisha Media Institute of Southern Africa, Tanzania chapter (Misa Tan), SIkIKA, kabla ya kurejea LHRC na kuongoza LHRC Online Public Database on Constitutional Resources. akiunga mkono umma na habari juu ya jinsi katiba ya Tanzania ilivyoandikwa, kutafsiriwa na kutekelezwa. Aliboresha mfumo wa usimamizi wa kidijitali kwa ajili ya usimamizi wa ushiriki wa umma na kituo cha rasilimali.[11]

  1. "Geline Fuko: Making a difference thanks to Erasmus Mundus". EEAS - European External Action Service - European Commission (kwa Kiingereza). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-22. Iliwekwa mnamo 2020-04-07.
  2. fpfis-admin (2017-01-27). "Dėmesio centre: programa „Erasmus+" atvira pasauliui". Erasmus+ - European Commission (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-04-07.
  3. "Geline Fuko: A promising leader who will work towards the betterment of Africa". Hamasa Magazine (kwa American English). 2018-05-12. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-02-22. Iliwekwa mnamo 2020-04-07.
  4. "LHRC | Katiba". katiba.humanrights.or.tz. Iliwekwa mnamo 2020-04-07.
  5. "Remarks by the President at the Young African Leaders Initiative Town Hall". whitehouse.gov (kwa Kiingereza). 2016-08-03. Iliwekwa mnamo 2020-04-07.
  6. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2018-06-22. Iliwekwa mnamo 2018-10-20.
  7. fpfis-admin (2017-01-27). "Dėmesio centre: programa „Erasmus+" atvira pasauliui". Erasmus+ - European Commission (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-04-07.
  8. 1 2 "Nakala iliyohifadhiwa" (PDF). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo (PDF) mnamo 2020-02-22. Iliwekwa mnamo 2020-04-07.
  9. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-08-03. Iliwekwa mnamo 2019-01-12.
  10. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-10-22. Iliwekwa mnamo 2019-01-12.
  11. "LHRC | Katiba". katiba.humanrights.or.tz. Iliwekwa mnamo 2020-04-07.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]