Uhasibu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Uhasibu
Uhasibu


Uhasibu (kwa Kiingereza: accounting) ni upimaji wa hali ya kifedha ya shirika au biashara. Baada ya upimaji huo, mhasibu ana jukumu la kuwasilisha taarifa kwa wanaohusika.

Mfumo wa uhasibu unaofanyika hivi leo ulianzishwa na mwanahisabati wa Italia kwa jina Luca Pacioli mwaka 1494. Uhasibu, ambao wengi huuita 'lugha ya biashara', hupima matokeo ya kiuchumi ya shirika na baadaye kuwajulisha washika dau. Anayefanya kazi ya uhasibu huitwa mhasibu.

Uhasibu unaweza kugawanywa mara tano:

  • Uhasibu wa kifedha (financial accounting)
  • Uhasibu wa kimeneja (management accounting)
  • Ukaguzi kutoka nje (external auditing)
  • Uhasibu wa ushuru (tax accounting)

Uhasibu wa kifedha[hariri | hariri chanzo]

Uhasibu wa kifedha ni utengenezaji wa ripoti kuhusu fedha za shirika fulani. Ripoti hizi hutumika na watu wa nje ambao wangependa kuwekeza katika shirika lile au kulikopea .

Uhasibu wa kimeneja[hariri | hariri chanzo]

Uhasibu huu hufanyika ili kuwezesha mameneja kufanya maamuzi kuhusu shirika.

Ukaguzi wa nje[hariri | hariri chanzo]

Ukaguzi wa nje au external auditing ni uhakiki kwamba yaliyofanywa na mhasibu ni kweli. Mahasibu wanaofanya ukaguzi wa nje huajirika na shirika kuja kufanya hesabu za hasibu wako kuona kwamba hakufanya makosa na hamna utapeli wowote isiende kuwa mhasibu wako akudanganya.

Uhasibu wa ushuru[hariri | hariri chanzo]

Uhasibu wa ushuru ni upimaji wa ushuru ambao shirika lafaa kulipa kwa serikali.

Kutafuta mhasibu anayefaa[hariri | hariri chanzo]

Mashirika mengi huwaza jinsi ya kutafuta mhasibu anayefaa katika shirika zao awafanyie hesabu na kuona kwamba pesa zinatumika sawa. Je, ni yapi wanafaa kuangazia wanapoajiri mhasibu:

Unapoajiri mhasibu, wafaa ufanye utafiti kwa wengine waliowaajiri ujue ni yupi anayefaa

Katika uhasibu kuna wale walio na uspesheli wa ushuru, umeneja, ukaguzi wa nje, mauzo au fedha. Ni vizuri uhakikishe kwamba yule ambaye unaajiri ana taaluma inayoendana na kazi unayotaka afanye. Pia ni vizuri umchague aliye na kisomo cha juu zaidi ikiwezekana kwa maana huenda akawa anayajua maswala ibuka katika taaluma ile na atakusaidia shirika lako lifuate maagizo yaliyoko kwenye nchi yako. Ukifanya hivi utampata yule aliye na best accountancy na atakusaidia katika kutatua yaliyopo kwenye shirika.

Mhasibu wako awe na tajriba au uzoefu mwingi wa kazi asiwe ametoka moja kwa moja chuoni.

Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Uhasibu kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.