Birisi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Typhlopidae)
Birisi
Birisi Mkubwa wa Schlegel (Afrotyphlops schlegelii)
Birisi Mkubwa wa Schlegel (Afrotyphlops schlegelii)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Reptilia (Wanyama wenye damu baridi na magamba ngozini)
Oda: Squamata (Mijusi, mijusi-nyungunyungu na nyoka)
Nusuoda: Serpentes (Nyoka)
Familia: Typhlopidae (Nyoka walio na mnasaba na birisi)
Merrem, 1820
Ngazi za chini

Nusufamilia 4:

Birisi ni nyoka wasio na sumu wa familia Typhlopidae. Kwa lugha nyingine huitwa “nyoka vipofu” mara nyingi, kwa sababu hawana macho au macho yamepunguka mpaka madoa meusi yanayoweza kulinganua nuru na giza tu. Spishi moja, birisi tingatinga, imeainishwa katika familia Xenotyphlopidae.

Nyoka hawa ni wafupi na wembamba, sm 95 kwa kipeo lakini sm 30-50 kwa kawaida. Spishi fupi sana ni birisi-Asia mdogo (sm 5-15) na huyu ni nyoka mfupi kabisa duniani. Rangi yao ni nyeusi, kijivu, kahawia au pinki pengine pamoja na madoa au mabaka.

Birisi huchimba ardhini, huingia vishimo au hujificha chini ya mawe au magogo, mara nyingi magogo yaliyooza. Kwa hivyo hawahitaji macho. Hula mchwa hasa.

Nyoka hawa hawana sumu na kwa kisa chochote mdomo wao ni mdogo sana; kwa hivyo hawawezi kung'ata mtu na wanaweza kukamatwa bila shida.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) A field guide to the Reptiles of East Africa. Academic Press, San Diego, CA, USA.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Birisi kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.