Tanzania Safari Channel

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Tanzania Safari Channel
Nembo ya Tanzania Safari Channel
Nembo ya Tanzania Safari Channel
Kutoka mji Dar es salaam
Nchi Tanzania
Eneo la utangazaji Kote duniani
Kituo kilianzishwa mwaka 2018
Mwenye kituo Televisheni ya Taifa ya Tanzania
Tovuti tanzaniasafarichannel.go.tz

Tanzania Safari Channel ni chaneli iliyo chini ya Televisheni ya Taifa ya Tanzania (TBC) iliyoanzishwa kwa lengo la kutangaza hifadhi na vivutio vya utalii nchini Tanzania.[1]

Tanzania Safari ilizinduliwa tarehe 15 Disemba 2018 [2][3] na waziri mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Ilianzishwa ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli alilolitoa alipozuru makao makuu ya shirika hilo Mei 16, 2019 ambapo aliagiza kuwepo kwa chaneli hiyo itakayokuwa inaonyesha vivutio vya utalii.[4]

Chaneli hii ilianzishwa kwa ushirikiano wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na wadau wengine wa utalii wakiwemo Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).

Mchakato wa kuanzisha chaneli hii ulihusisha pia mikutano na wadau wa sekta binafsi ambao shughuli zao zinahusiana na masuala ya utalii.

Chaneli hii inapatikana kwenye ving'amuzi mbalimbali ikiwa ni pamoja na StarTimes na Azam TV.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]