Steven Gerrard

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Steven Gerrard

Steven George Gerrard (alizaliwa tarehe 30 Mei 1980) ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu kutoka Uingereza, timu ya Liverpool F.C., nafasi ni kiungo wa kati. Pia alikuwa nahodha wa timu hiyo na hata wa timu ya taifa.

Kwa sasa ni meneja, mfanyakazi wa akademi hiyo. Kwa sasa ni mtangazaji wa mpira wa miguu kwenye kituo cha BT Sport's.

Akitambulika kuwa kiungo bora kwa kipindi alichokuwa akicheza, Gerrard alipewa tuzo ya mchezaji bora wa UEFA ngazi ya klabu, 2005 akiwa mshindi wa tatu kwenye kinyang'anyiro cha mchezaji bora wa dunia. Mwaka 2009 Zinedine Zidane na Pelè walimchagua kuwa mchezaji bora wa dunia. Gerrard alikuwa na sifa ya kuwa na kiwango kizuri uwanjani hata kwenye uongozi, Gerrard ni mchezaji wa kwanza kushinda goli kwenye fainali za FA Cup, fainali za kombe la ligi na fainali za UEFA na kushinda kwenye kila fainali. Gerrard ndiye mwanasoka pekee aliyefunga katika Fainali ya Kombe la FA, Fainali ya Kombe la Ligi, Fainali ya Kombe la UEFA na Fainali ya Ligi ya Mabingwa ya UEFA, akishinda kila hafla.

Alhaj Diof aliwahi kumtuhumu nahodha huyo wa Liverpool na Uingereza kwa kuonesha ubaguzi waziwazi kwa kusema Ligi ya Uingereza ni kwa ajili ya Wazungu sio ya Waafrika.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Steven Gerrard kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.