Tiwa Savage

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Savage (rapper))
Tiwa Savage akiwa jukwaani

Tiwatope Savage (anayejulikana kama Tiwa Savage; amezaliwa 5 Februari 1980) ni mwimbaji, mwandishi wa nyimbo na mwigizaji wa nchini Nigeria.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Alizaliwa Isale Eko, alihamia London akiwa na umri wa miaka 11 ili kujiunga na sekondari. Miaka mitano baadaye, alianza kazi yake ya muziki akiimba nyimbo za wasanii kama George Michael na Mary J. Blige. Baada ya kushiriki shindano la The X Factor la Uingereza na kuhitimu kutoka Chuo cha Muziki cha Berklee, Savage alisaini mkataba na Sony / ATV mnamo 2009. Alichochewa na ukuaji wa tasnia ya muziki ya Nigeria, Savage alirudi Lagos na kusaini mkataba na Mavin Records mnamo 2012. Alitokea kwenye label ya albamu ya mkusanyiko ya 2012 Solar Plexus.

Albamu yake ya kwanza ilitolewa Julai 3, 2013. Iliungwa mkono na nyimbo saba: "Kele Kele Love", "Love Me (3x)", "Without My Heart", "Ife Wa Gbona", "Folarin", "Olorun Mi" and "Eminado". Albamu ya pili ya studio ya Savage R.E.D ilitolewa Desemba 19, 2015. Iliambatana na nyimbo mbili: "My Darlin" and "Standing Ovation". Juni 2016, Savage alisaini usimamizi wa Roc Nation. Septemba 2017, aliachilia ''Sugarcane''. Iliungwa mkono pia na single mbili:"All Over" na "Ma Lo". Mei 2019, alitangaza kujiunga na Universal Music Group na kutoka kwa Mavin Record.

Savage anaimba kwa Kiingereza na Kiyoruba. Mchango wake katika tasnia ya muziki ya Nigeria umepata mafanikio kadhaa, pamoja na Tuzo mbalimbali za Muziki.

Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tiwa Savage kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.