Sakramentari

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ukurasa wa Tyniec Sacramentary, National Library of Poland.[1]

Sakramentari (kwa Kilatini "Sacramentarium" kutoka neno "sacramentum", yaani sakramenti) ni kitabu kimojawapo cha liturujia, hasa ya Kanisa la Kilatini.

Yaliyomo ni hasa sala inayotakiwa kusomwa au kuimbwa na askofu au padri katika Misa na ibada nyingine kadhaa, si masomo wala maneno yanayotakiwa kusomwa au kuimbwa na wengine.[2] Sehemu hizo zimo katika vitabu vingine, kama Kitabu cha Injili, Kitabu cha masomo na Graduale.[2]

Sakramentari kadhaa za zamani, hasa za mapokeo ya Roma, zinapatikana hadi leo, ama nzima ama sehemu tu. Maarufu zaidi ni zile zinazoitwa Leonianum, Gelasianum na Gregorianum.[2]

Umuhimu wake ulipungua vitabu vyote vya Misa vilipounganishwa katika misale za Karne za Kati.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Oskar Halecki; W: F. Reddaway; J. H. Penson (1950). The Cambridge History of Poland. Cambridge University Press. p. 68. ISBN 1-00-128802-5. 
  2. 2.0 2.1 2.2 Catholic Encyclopedia, s.v. Liturgical Books
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sakramentari kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.