Párvusz

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

'

Párvusz
Amezaliwa1 Machi 1981 (1981-03-01) (umri 43)
NchiHungarian
Kazi yakeKuchora


Párvusz (alizaliwa kama Norbert Kiss, Budapest, Hungaria, mnamo tarehe. 1 Machi mwaka1981) ni msanii wa uchoraji picha kutoka nchini Hungaria. Amesomea mambo haya mjini Budapest na Szeged. Yeye ni Mkristo, hivyo Wakristo wengi hutumia picha zake katika maigizo.

Staili na kazi zake[hariri | hariri chanzo]

Staili yake kubwa ni ile ya kutumia wino mweusi wa Kihindi. Pia kuna kipindi hutumia rangi za maji, lakini kikawaida hufanya kazi zake kwa kutumia staili moja tu ya picha yaani rangi nyeupe na nyeusi. Watu mashuhuri wa Kihungaria Endre Szász na Dutch M. C. Escher wameona kazi zake. Staili hii ilizaliwa mnamo mwaka 2004, tabia kuu anayoitumia kuchora picha zake ni kutengeneza miraba kadhaa na kuichanganya pamoja. Moja kati ya kazi zake za mwanzoni ni pamoja na ile iliyokuwa ikiitwa Homeland ya mwaka 2004. Mnamo mwaka 2009 amenza kutumia kwenye vibao.

Kuna badhi ya kazi zake zimeshwahi kutumia kwenye maonyesho huko nchini Norway.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]