Ol Doinyo Lengai

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ol Doinyo Lengai wakati wa mlipuko wake wa 1966.
Ol Doinyo Lengai kutoka ziwa Natron.

Ol Doinyo Lengai (maana kwa Kimaasai ni "Mlima wa Mungu") ni mlima wenye asili ya volkeno katika Tanzania ya Kaskazini. Iko takriban km 120 kaskazini-magharibi kwa Arusha na km 25 kusini kwa Ziwa Natron.

Mlima una kimo cha m 2690 juu ya UB.

Ni volkeno ya pekee duniani kutokana na aina ya lava yake inayotoka hali ya kiowevu (majimaji) lakini si moto sana (mnamo 500° - 600 °C).

Ol Doinyo Lengai ililipuka tena kuanzia Machi 2006. Katika mwaka 2007 mlima umesababisha mitetemeko ya ardhi ya mara kwa mara kuanzia tarehe 12 Julai. Tetemeko la tarehe 18 Julai lilisikika hadi Nairobi.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]