Nyoka-chale

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nyoka-chale
Nyoka-chale Madoadoa (Homoroselaps lacteus)
Nyoka-chale Madoadoa (Homoroselaps lacteus)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Reptilia (Wanyama wenye damu baridi na magamba ngozini)
Oda: Squamata (Mijusi, mijusi-nyungunyungu na nyoka)
Nusuoda: Serpentes (Nyoka)
Familia: Lamprophiidae (Nyoka walio na mnasaba na chata)
Fitzinger, 1843
Nusufamilia: Atractaspidinae (Nyoka wanaofanana na nyoka wachimbaji)
Günther, 1858
Jenasi: Homoroselaps
Ngazi za chini

Spishi 2:

Nyoka-chale ni nyoka wenye sumu wa jenasi Homoroselaps katika familia Lamprophiidae. Wamepewa jina hili kwa sababu ya milia yao ya rangi nzuri. Wanatokea Afrika ya Kusini.

Nyoka hawa ni wafupi na wembamba, sm 65 kwa kipeo lakini sm 20-40 kwa kawaida. Wana mlia njano au mwekundu kwa urefu mzima wa mgongo na milia myeusi au mabaka meusi mbavuni.

Nyoka-chale hupumzika katika vichuguu na kuwinda kati ya manyasi na katika takataka za majani ambapo hukamata mijusi (mijusi bila miguu hasa) na nyoka wengine wadogo kama birisi.

Chonge ni meno ya nyuma. Nyoka hawa wanaweza kung'ata lakini sumu siyo hatari sana. Hata hivyo inaweza kusababisha kufura na maumivu makali ya kichwa.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) A field guide to the Reptiles of East Africa. Academic Press, San Diego, CA, USA.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nyoka-chale kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.