Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (kwa Kiingereza Order of Mwalimu Julius Kambarage Nyerere) ni tuzo ya heshima zaidi nchini Tanzania.[1]. Tuzo hiyo ilipewa jina hilo ili kumuenzi rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Tuzo hiyo ilianzishwa na Jakaya Mrisho Kikwete mnamo Desemba 2011, wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bara, ambayo kabla ya hapo ilikuwa ikijulikana kama Tanganyika.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. "Rais Kikwete atibua nyongo" [President Kikwete awards medals] (kwa Swahili). MwanaHalisi. 21 December 2011. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2017-02-23. Iliwekwa mnamo 13 October 2013.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)