Neli (ndege)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Neli
Neli kijani
Neli kijani
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Passeroidea
Familia: Nectariniidae (Ndege walio na mnasaba na chozi)
Vigors, 1825
Ngazi za chini

Jenasi 3, spishi 22:

Neli ni ndege wadogo wa jenasi kadhaa katika familia Nectariniidae. Spishi hizi ni kama chozi lakini kubwa kuliko spishi nyingi za chozi. Takriban spishi zote zina rangi ya majani. Manyoya ya kati ya mkia ni marefu sana katika spishi za Nectarinia. Domo lao limepindika na hutumika kwa kutoa mbochi katika maua au wadudu katika matundu. Hula mbochi hasa na pengine maji ya matunda na wadudu pia. Ndege hawa wanatokea Afrika kusini mwa Sahara. Tundu lao lina umbo la mfuko na limening'izika kwa vitawi vyembamba. Jike hutaga mayai 2-4.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]