Nathaniel Borenstein

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Nathaniel S. Borenstein (alizaliwa tar. 23 Septemba 1957 ) ni mwanasayansi wa kompyuta wa Marekani . Yeye ni mmoja wa wabunifu wa protoko ya MIME kwa ajili ya barua pepe za kielektroniki mtandaoni . [1]

Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Borenstein alipata Shahada ya sanaa katika Hisabati na Masomo ya Kidini kutoka Chuo cha Grinnell mwaka wa 1980, na Ph.D katika Sayansi ya Kompyuta kutoka Chuo Kikuu cha Carnegie Mellon mwaka 1985. Hapo awali alisoma Chuo Kikuu cha Jimbo la Ohio (1974-75), Chuo cha Deep Springs, California (1975-76), na Chuo Kikuu cha Kiebrania cha Jerusalem, Israel (1978-79). [2] Akiwa CMU, alishiriki kutengeneza sehemu ya barua pepe ya Mradi wa Andrew . Mfumo wa Ujumbe wa Andrew ulikuwa mfumo wa kwanza wa barua pepe wa mtandaoni kutumika nje ya maabara. Mnamo 1989 alikua mwanachama wa wafanyikazi wa kiufundi huko Bellcore (Watafiti wa Mawasiliano ya Bell). Huko alitengeneza mifumo mbali mbali ya barua pepe. Alikua na jukumu la kutuma kiambatisho cha kwanza cha barua pepe cha MIME mnamo Machi 11, 1992.

Borenstein alikuwa mwanzilishi wa First Virtual Holdings mwaka wa 1994, inayoitwa "cyberbank" na Smithsonian Institution, na NetPOS.com mwaka wa 2000. Alifanya kazi IBM kama mhandisi mashuhuri Cambridge, Massachusetts . Kisha akawa mwanasayansi mkuu katika kampuni ya usimamizi wa barua pepe Mimecast mnamo Juni 2010. [3]

Maisha binafsi[hariri | hariri chanzo]

Borenstein anaishi na mke wake, Trina, huko Ann Arbor na Greenbush, Michigan ; wana watoto wanne, na wajukuu watano. [4]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. NSB Home Page. web site, including CV. Iliwekwa mnamo May 3, 2011.
  2. NSB Home Page. web site, including CV. Iliwekwa mnamo May 3, 2011.
  3. "Human Capital: People on the Move", Boston Business Journal. Retrieved on May 3, 2011. 
  4. NSB Home Page. web site, including CV. Iliwekwa mnamo May 3, 2011."NSB Home Page". web site, including CV