Naomba Kwako Bibiye

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
"Naomba Kwako Bibiye"
"Naomba Kwako Bibiye" kava
Wimbo wa Ikhwani Safaa Musical Club

kutoka katika albamu ya A Hundred Years Of Taarab In Zanzibar

Umetolewa 1984/1985
Aina ya wimbo Taarab asilia
Urefu 12:28
Mtunzi Maulid Machaprara
Mtayarishaji Malindi
A Hundred Years Of Taarab In Zanzibar orodha ya nyimbo
  1. Vingaravyo Vyote Si Dhahabu
  2. Cheo Chako
  3. Hofu Yako Iondoe
  4. Waache Waseme
  5. Zinduna
  6. Mpenzi Wangu Hawezi
  7. Pendo Kitu Cha Hiyari
  8. Naomba Kwako Bibiye

"Naomba Kwako Bibiye" ni jina la wimbo ulioimbwa na kundi zima la muziki wa taarab kutoka mjini Zanzibar, Ikhwani Safaa Musical Club au Malindi. Wimbo umetoka miaka ya 1980 na kuimbwa na marehemu Maulid Mohamed Machaprara. Wimbo unatoka katika albamu ya kompilesheni ya "A Hundred Years Of Taarab In Zanzibar". [1] Kompilesheni hii ilitazama nyimbo za Malindi tangu kuanzishwa kwake kuanzia 1905 hadi 2005. Wimbo huu ni wa 8 kutoka katika albamu hii. Machaprara anamlilia mpenzi wake anayejitia kisebusebu juu ya mapenzi yake kwake. Anambembeleza amtie mwake moyoni, kwani mengi ni mateso ashuhudiayo duniani hapa. Haishi hapo, ameonjeshwa raha ya mtu anayependwa, mbaya zaidi akamfanyia hila ya mapenzi.

Maudhui[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]