Mugo Kibati

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mugo Kibati

Mugo Kibati amezaliwa mwaka 1969 nchini Kenya ni Meneja wa Biashara ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Telkom Kenya, kampuni ambayo inatoa huduma kamili za mawasiliano ya simu, sauti na data, zinazotolewa katika sekta ya ushirika, serikali na SME.[1]

Kibati pia ni Mwenyekiti wa Kituo cha Umeme wa Upepo cha Ziwa Turkana (LTWP), kampuni yenye ekari 40,000 (162km2) za ardhi, inauwezo wa kuzalisha umeme wa MW 301, ina mitambo 365 na gharama ya mtaji ni Ksh 76 bilioni (€623 milioni). LTWP ndio kampuni kubwa zaidi ya nishati ya upepo barani Afrika.[1]

Kibati pia amefanya kazi katika mashirika kadhaa, ikiwemo benki ya I&M na Kikundi cha Apollo. Pia amekuwa na nafasi ya juu ya uongozi wa sekta ya kitaifa katika Umoja wa Wafanyabiashara wa Kenya, Chama cha Wafanyabiashara wa Kenya (KAM) na Umoja wa Sekta binafsi wa Kenya (KEPSA). Pia alihudumu katika Baraza la Wabunge na kuongoza Chama cha Wavulana Wazee kaika chuo kikuu cha Alliance kwa miaka kadhaa.

Maisha ya awali na Elimu[hariri | hariri chanzo]

Alilelewa katika mji wa Nakuru na Mombasa, Kibati alihitimu katika Chuo Kikuu cha Moi mwaka 1991, ana shahada ya Teknolojia pamoja na Digrii ya Uhandisi wa Umeme. Ana Shahada ya Uzamili ya Sayansi katika Teknolojia na Sera, kutoka katika Taasisi ya Teknolojia ya Massachusetts (MIT). [2] Programu ya Teknolojia na Sera (TPP) huko MIT inashughulikia changamoto za kijamii ... katika mstari wa teknolojia na sera, kuhamasisha sayansi na uhandisi ili kuwasilisha mikakati na sera zenye busara, zinazolenga kunufaisha jamii hadi ngazi ya kimataifa.

Sifa nyingine ya Kibati ni pamoja na Digrii ya Utawala wa Biashara katika Chuo Kikuu cha Biashara cha George Washington. Pia ana Shahada ya Uchumi katika Uchumi wa Umoja wa Ulaya kutoka katika Chuo Kikuu cha St Peters, nchini Uingereza.[2]

Kazi[hariri | hariri chanzo]

Mhandisi kwa ajili ya mafunzo, Kibati alifanya kazi katika Teknolojia ya Lucent, nchini Marekani katika nafasi ya Meneja Masoko wa Kiufundi. Pia alifanya kazi katika Kampuni ya Bamburi Cement (Lafarge Copee) kuanzia Novemba 1991 hadi Mei 1997 na kufuata kazi yake ya awali katika kiwanda cha kusafisha mafuta cha Kenya Petroleum Refineries huko Mombasa, Kenya.[2]

Kuanzia mwaka 2004 Kibati alihudumu kama Mkurugenzi Mkuu na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Cables kwa miaka minne hadi Juni 2008.[3] Katika kipindi hicho, kampuni ilitumia mkakati uliofanikiwa katika usambazaji na ukuaji, na kuongeza mapato ya kila mwaka kutoka KSh. milioni 400 hadi Ksh. bilioni 3.5, faida kutoka kwa KSh. milioni 15 hadi Ksh. milioni 600 na thamani ya hisa ya soko ya kampuni kutoka KSh. milioni 600 hadi KSh. bilioni 12. Mkakati huo ulihusisha ushirikiano wa kimkakati uliojadiliwa na kampuni inayoongoza duniani kwa kutengeneza nyaya na upatikanaji wa vifaa vya utengenezaji nchini Tanzania na Afrika Kusini. Mwisho wa utawala wake, kampuni imefikia hali ya 'blue chip' na vile vile bei ya hisa inayokuwa kwa kasi zaidi katika Soko la Hisa la Nairobi mwaka (2005/2006) ikilinganishwa na wajibu wa uwazi wa kisheria.[4]

Mnamo Julai 2009, Kibati alichaguliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Maono ya Kenya 2030. Katika jukumu hilo, Kibati aliongoza utekelezaji wa Maono ya Kenya 2030, mkakati rasmi wa kitaifa wa kubadilisha Kenya kuwa nchi mpya kiviwanda ifikapo mwaka wa 2030. Wakati wa utumishi wake, Kibati, akiungwa mkono na wafanyakazi wenzake serikalini, sekta binafsi na mashirika ya kiraia, aliweka msingi wa mabadiliko ya kitaifa yaliyopangwa. Pia anasifiwa kwa kuwakusanya washiriki mbalimbali kuelekea makubaliano juu ya njia ya ukuaji wa uchumi na maendeleo ya kijamii. Aliacha jukumu hilo mnamo Oktoba 2013.[3]

Mnamo Februari 2015, Kibati alijiunga na Sanlam Kenya (wakati huo PanAfrica Insurance), kampuni ya bima na uwekezaji na mwanachama wa Kundi la Sanlam la Afrika Kusini, kama Mkurugenzi Mkuu.[5][6] Alishikilia wadhifa huu hadi Machi 2018.

Mnamo Februari 2016, Kibati alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa M-kopa Sola, jukumu hilo alilishikilia hadi Novemba 2018. Kampuni imeunganisha nishati ya jua zaidi ya nyumba 600,000 kwa bei nafuu, na nyumba mpya 500 zikiongezeka kila siku. [7]

Tangu 2017, Kibati aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kituo cha Umeme wa Upepo cha Ziwa Turkana (LTWP). Ilikamilishwa Januari 2017, shamba la nishati ya upepo la ekari 40,000, ndiyo uwekezaji mkubwa wa ndani nchini Kenya tangu uhuru wake, na ndiyo kampuni kubwa zaidi ya nishati ya upepo katika historia ya Afrika hadi sasa.[8]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 Bonface Otieno (9 November 2018). "Telkom Appoints Mugo Kibati As CEO". Business Daily Africa. Nairobi. Iliwekwa mnamo 1 November 2019.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  2. 2.0 2.1 2.2 Capital FM Correspondent (9 November 2018). "Telkom Kenya appoints Mugo Kibati its new CEO". Nairobi: 98.4 Capital FM. Iliwekwa mnamo 9 November 2018.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  3. 3.0 3.1 Capital FM (15 October 2013). "Mugo Kibati confirms exit from Vision 2030 Secretariat". Nairobi: 98.4 Capital FM. Iliwekwa mnamo 9 November 2018.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  4. Juma, Victor (16 July 2015). "East African Cables CEO resigns after 7 years at the helm". Business Daily Africa. Nairobi. Iliwekwa mnamo 9 November 2018.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  5. Juma, Victor (3 February 2018). "Sanlam Kenya CEO Mugo Kibati set to leave at end month". Business Daily Africa. Nairobi. Iliwekwa mnamo 9 November 2018.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  6. Juma, Victor (25 February 2018). "Mugo Kibati appointed new CEO of Pan Africa Insurance". Business Daily Africa. Nairobi. Iliwekwa mnamo 9 November 2018.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  7. Guguyu, Otiato (16 March 2016). "M-Kopa hires Mugo Kibati as board chair". Daily Nation. Nairobi. Iliwekwa mnamo 9 November 2018.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  8. Capital FM (22 October 2018). "Lake Turkana Wind Power project to connect 365 turbines to the grid". Nairobi: 98.4 Capital FM. Iliwekwa mnamo 9 November 2018.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)