Mtiti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtiti
Mtiti wa Afrika
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Strigiformes (Ndege kama bundi)
Familia: Strigidae (Ndege walio na mnasaba na bundi)
Nusufamilia: Striginae (Ndege wanaofanana na bundi)
Jenasi: Margarobyas Olson & Suárez, 2008

Megascops Kaup, 1848
Otus Pennant, 1769
Psiloscops Coues, 1899 Ptilopsis Kaup, 1848 Pyrroglaux Yamashina, 1938

Spishi: Angalia katiba

Mititi au vilio ni ndege mbuai wa jenasi mbalimbali katika familia Strigidae. Kwa kawaida ndege hawa ni wadogo kuliko bundi (sm 16-30) na wana rangi ya kahawa au kijivu pamoja na madoadoa ambayo yanafanana na gome la miti. Kwa kawaida jike ni mkubwa kuliko dume. Mititi hula wadudu hasa lakini watambaazi, wanyama na ndege wadogo pia na hata nyungunyungu na amfibia. Huwinda usiku kwa kawaida. Jike huyataga mayai 2-6 katika shimo lililoachwa na ndege au mnyama mwingine, lakini mara nyingi kinda moja tu akua.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]