Mkonokono

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mstafeli-mwitu)
Mkonokono
(Annona senegalensis)
Makonokono
Makonokono
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Magnoliids (Mimea ambayo maua yao yana mizingo ya tepali tatu na chavua yenye kitundu kimoja)
Oda: Magnoliales (Mimea kama mparachichi)
Familia: Annonaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mkonokono)
Jenasi: Annona
L.
Spishi: A. senegalensis
Pers.

Mkonokono ni mti mdogo wa familia Annonaceae. Matunda yake yanayolika huitwa makonokono. Spishi hii ina majina mengi mengine, k.m. mbokwe, mchekwa, mtomoko-mwitu, mtopetope-mwitu na mstafeli-mwitu. Mti huu una maua madogo njanokijani yenye petali nene. Matunda yana umbo wa yai na rangi ya manjano yakiwa yaliyoiva. Nyama ni njano hadi machungwa yenye ladha tamu. Mbegu nyeusi ni kubwa kiasi.

Picha[hariri | hariri chanzo]