Mitishamba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Basil, majani ya kawaida ya upishi.

Mitishamba ni mimea inayothaminiwa kama dawa[1]. Katika matumizi ya dawa, inawezekana kutumia sehemu yoyote ya mmea, ikiwa ni pamoja na majani, mizizi, maua, mbegu, gundi, maganda ya mizizi, maganda ya ndani, nafaka na mara nyingine matunda au sehemu nyingine za mmea.

Matumizi[hariri | hariri chanzo]

Mimea ina kemikali aina ya phytochemicals ambayo ina athari kwa mwili. Katika historia, kutoka katika Bibilia, Kurani, mashairi ya Siddhar kutoka Tamils, Vedas na maandiko mengine ya zamani, faida za mitishamba za dawa zimetajwa.

Kunaweza kuwa na athari kidogo inapotumiwa katika kiasi kidogo kama vile "kuunga" kwenye upishi, na baadhi ya mitishamba huwa sumu ikitumiwa kwa kiasi kikubwa. Kwa mfano, baadhi ya aina za mitishamba, kama vile dondoo ya St John's-Wort Hypericum perforatum au ya Kava Piper methysticum yanaweza kutumika kwa madhumuni ya matibabu ya unyogovu na kupunguza fikira. Hata hivyo, kiasi kikubwa cha mitishamba hii inaweza kusababisha sumu, na lazima itumike kwa hadhari. Dutu moja inayofanana na mitishamba, iitwayo Shilajit inaweza hasa kusaidia kupunguza vipimo vya sukari kwenye damu ambako ni muhimu hasa kwa wale wanaosumbuliwa na kisukari. Mitishamba kwa muda mrefu imekuwa ikitumika kama msingi wa Madawa ya mimea ya Kichina na imetumiwa tangu karne ya 1 BK

Baadhi ya mitishamba hutumika sio tu kwa matumizi ya upishi na dawa, lakini pia kwa madhumuni ya burudani; mmea mmoja wa aina hii bangi.

Mitishamba ya upishi[hariri | hariri chanzo]

Matumizi ya neno "mitishamba" katika upishi kawaida hutofautisha kati ya mitishamba, na sehemu za mmea zenye majani ya kijani, na viungo, kutoka kwa sehemu nyingine za mimea, ambazo ni pamoja na mbegu, nafaka, ganda, mizizi na matunda. Mitishamba ya upishi hutofautishwa na mboga kwa kuwa, kama viungo, hutumika katika kiasi kidogo na hutoa ladha kuliko dutu kwa chakula.

Mitishamba mingi ya upishi huwa kwa zaidi ya misimu miwili kama vile zaatari au Lavender, wakati mingine ikikua kwa miaka miwili kama vile parsley au ya mwaka mmoja kama vile rehani (basil), na mingine baadhi ni vichaka (kama vile Rosemary, Rosmarinus officinalis), au miti (kama bay Laurel, Laurus nobilis) hii inatofautiana na mitishamba ya botania, ambayo kwa ufafanuzi haiwezi kuwa na mbao mimea. Baadhi ya mimea hutumiwa kama viungo au mitishamba, kama vile mbegu na gugu la Dill au mbegu na majani ya mgiligilani (dania, coriander leaves). Pia, kuna baadhi ya mimea kama wale katika familia naana (mint) ambayo hutumiwa kwa matumizi ya upishi na vilevile dawa.

Mitishamba Mitakatifu[hariri | hariri chanzo]

Mitishamba hutumika katika dini nyingi - kama vile katika manemane ya Ukristo na ubani ambayo ilitumika kuheshima wafalme. (Commiphora myrrha), mzizi wa ague (Aletris farinosa) (Boswellia spp)) na katika Anglo-Saxon pagan Nine Herbs Charm. Watamil huabudu Mwarobaini unaoitwa Vempu (Kitamil: வேம்பு). Katika Uhindi aina ya Basil iitwayo Tulsi au Basil Takatifu huabudiwa kama mungu mke kwa thamani yake ya dawa tangu nyakati za Vedic. Wahindu wengi wana mmea wa Tulsi mbele ya nyumba zao. Waumini wa imani ya Rastafari na imani mbalimbali nchini India kuchukulia bangi kuwa mmea takatifu uliopewa mtu na mungu

Waganga wa Siberia pia alitumia dawa kwa madhumuni ya kiroho. Madawa na mimea vimetumika duniani kote kwa mambo ya kiroho.

Kudhibiti wadudu[hariri | hariri chanzo]

Mitishamba pia inajulikana miongoni mwa wakulima kwa umuhimu wake katika kudhibiti wadudu. Mint, spearmint, peppermint, na pennyroyal ni baadhi ya mitishamba hii. Mitishamba hii ikipandwa kuzunguka msingi wa nyumba inaweza kusaidia kufukuza wanyama na wadudu kama nzi, panya, mdudu chungu, chawa, nondo na kupe miongoni mwa wengine. Haijulikani kuwa na madhara au hatari kwa watoto au vipenzi, au vitu vyovyote vya nyumbani

Mitishamba ya botania[hariri | hariri chanzo]

Katika botania matumizi ya jina mitishamba ina maanisha mmea wowote usio na mbao, bila kujali ladha yake, uturi au mali nyingine. Mitishamba ya botania hivyo haiwezi kuwa mmea wowote wenye mbao kama vile mti au shrub.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Dictionary.com. Iliwekwa mnamo 2007-12-19.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Jua habari zaidi kuhusu Mitishamba kwa kutafuta kupitia mradi wa Wikipedia Sister
Uchambuzi wa kamusi kutoka Wikamusi
Vitabu kutoka Wikitabu
Dondoo kutoka Wikidondoa
Matini za vyanzo kutoka Wikichanzo
Picha na media kutoka Commons
Habari kutoka Wikihabari
Vyanzo vya elimu kutoka Wikichuo
Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mitishamba kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.