Mick Pearce

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mick Pearce (Alizaliwa 2 Juni 1938) ni msanifu wamajengo nchini Zimbabwe.

Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Pearce alizaliwa mnamo June 2 1938, huko Harare.[1] Alitunukiwa shahada katika chuo kikuu cha Architectural Association School of Architecture huko London mwaka 1962. Amefanya miradi nchini UK, Zambia, Zimbabwe, Australia, China na pia Afrika Kusini.[1]

Katika miaka 20 iliyopita, Pearce ameangazia usanifu endelevu na amechunguza kanuni za biomimicry,ambayo ni utambulisho wa mchakato wa asili na matumizi ya vifaa vya asili. Moja ya malengo ya mtindo wake wa usanifu ni kupunguza uharibifu wa mazingira. Pearce, anapendelea kutumia vifaa vya ndani na teknolojia za jadi kama vile vinu vya upepo (windmill).[1][2]


Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 1.2 Architects of Change. Biography Archived 21 Julai 2018 at the Wayback Machine.
  2. Architects for Peace. Excerpt from the jury report Archived 13 Septemba 2019 at the Wayback Machine. of the 2003 Prince Claus Award, presented to Mick Pearce on 10 Dec 2003