Mfyulisi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mfyulisi
(Prunus persica)
Kiunga cha mifyulisi
Kiunga cha mifyulisi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Rosids (Mimea kama mwaridi)
Oda: Rosales (Mimea kama mwaridi)
Familia: Rosaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mwaridi)
Nusufamilia: Amygdaloideae (Mimea iliyo na mnasaba na mlozi)
Jenasi: Prunus
L.
Nusujenasi: Amygdalus
(L.) Focke
Spishi: P. persica
(L.) Batsch, 1801

Mfyulisi ni mti mdogo wa jenasi Prunus (nusujenasi Amygdalus) katika familia Rosaceae. Matunda yake huitwa mafyulisi na haya yana ngozi yenye manyoya mafupi kama mahameli.

Asili ya mti huu ni Uchina, lakini sikuhizi unapandwa kila mahali katika kanda za nusutropiki.

Kuna aina mbili zenye matunda yaliyo na kifano kingine:

Mnektarini (var. nucipersica au var. nectarina) - ngozi ya matunda bila manyoya
Mfyulisi-donati (var. platycarpa) - matunda yenye umbo wa donati

Picha[hariri | hariri chanzo]