Mario Balotelli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mario Balotelli
Youth career
2001–2006Lumezzane
2006–2007Internazionale
Senior career*
MiakaTimuApps(Gls)
2006Lumezzane2(0)
2007–Internazionale47(15)
Timu ya Taifa ya Kandanda
2008–Italy U-2115(6)
* Senior club appearances and goals counted for the domestic league only and correct as of 5 Desemba 2009.

† Appearances (Goals).

‡ National team caps and goals correct as of 13 Novemba 2009
Mario Balotelli

Mario Barwuah Balotelli (amezaliwa 12 Agosti 1990) ni mwanakandanda wa Kiitalia.

Anajulikana sana kwa kasi yake na uwezo wa kiufundi. Balotelli, wakati mwingine hupewa jina Super Mario na watangazaji, anaweza kucheza sehemu yoyote katika safu ya kushambulia, lakini sanasana kama mshambuliaji mkuu. Yeye anajua kuipiga 'free-kick" na anaonwa na wengi kama mmoja wa wanakandanda wa Kiitaliano mwenye ahadi na matarajio kwa siku zinazokuja.

Maisha ya awali[hariri | hariri chanzo]

Balotelli alizaliwa kwa wavyele ambao walikuwa wahamiaji kutoka nchi ya Ghana, Thomas na Rose Barwuah katika mji mkuu wa Kiitaliano wa Palermo. Familia hii ilihamia Bagnolo Mella katika mkoa wa Brescia, Lombardy muda mfupi baada ya kuzaliwa kwa Balotelli. Mwaka wa 1993, akiwa na umri wa mika tatu, familia ya Barwuah ilikubali kuipatia familia ya Balotelli Mario huku hatua za kisheria zikipitishwa rasmi na Mahakama ya Brescia. Balotelli baadaye aliwashtaki wazazi wake waliomza kwa kosa la "uwindaji wa utukufu", na kusema kwamba wao walimtaka tu kwa sababu ya umaarufu wake. Wanaishi katika mji wa Concesio katika sehemu ya Brescia. Kulingana na Sheria ya 91 ya 5 Februari 1992, Balotelli alibidi kusubiri hadi siku yake ya kuzaliwa ya 18 ili apeane ombi la uraia wa Kiitaliano, kwani kupeanwa kwake kwa familia ya Balotelli haikuwa kamili, lakini alipata uraia huo rasmi tarehe 13 Agosti 2008.

Wasifu wa Klabu[hariri | hariri chanzo]

Lumezzane[hariri | hariri chanzo]

Balotelli alianza wasifu wake na klabu ya Lumezzane. Akiwa na umri wa miaka 15, alipandishwa ngazi hadi kwa timu kuu, na kucheza mechi yake ya kwanza ya ligi ya Serie C1 dhidi ya Padova.

Internazionale[hariri | hariri chanzo]

Internazionale walimsaini Balotelli kwa mkopo pamoja na chaguo la kumnunua mwaka wa 2006. Alianza katika kikosi chao cha vijana wasiozidi umri wa miaka 17 kisha alijiunga na timu ya vijana wasiozidi umri wa miaka 20 ya Primavera akiwa na umri wa miaka 16. Alifunga mkwaju wa penalti lililovunja sare ya 0-0 katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Sampdoria katika fainali ya ligi ya Primavera na alivua sifa kutoka kwa watu pamoja na mwenyekiti wa Inter Massimo Moratti.

Balotelli alicheza mechi yake ya kwanza ya timu kuu mnamo Desemba 2007, kwa kuingia kama mbadala wa David Suazo katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Cagliari. Siku tatu baadaye, alianzishwa katika mechi ya Coppa Italia dhidi ya Reggina na alifunga mabao mawili katika ushindi wa 4-1. Balotelli alipata usikivu wa kitaifa baada ya kufunga mabao mawili dhidi ya Juventus katika mechi ya marudiano ya robo-fainali ya Coppa Italia , kwa kusisimua katika ushindi wa Nerazzurri wa 3-2 ugenini. Bao lakek la kwanza la Serie A lilikuja mwezi Aprili mwaka wa 2008 katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Atalanta ugenini. Inter iliendelea na matokeo bora na hatimaye kushinda scudetto-ligi ya Kiitaliano- msimu wa 2007-08. Balotelli alikuwa mbadala katika fainali ya Supercoppa Italiana mwaka wa 2008 dhidi ya AS Roma. Aliingia kama mbadala wa Luis Figo, na kufunga bao katika dakika ya 83. Inter iliishinda fainali hiyo kupitia mikwaju ya penalti kwa mabao 6 kwa 5 baada ya mechi kumkamilika kwa sare ya 2-2.

Kabla ya kuanza kwa msimu wa 2008-09 Balotelli alisaini mkataba wa miaka mitatu na Inter. Mnamo Novemba 2008, alifunga bao lake la kwanza la Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya{ /0}, dhidi ya upande wa Cypriotiska Anorthosis Famagusta na kuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi wa Inter kufunga bao katika Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Akiwa na umri wa miaka 18 na siku 85 alivunja rekodi ambayo awali ilikuwa inashilikiwa na Obafemi Martins alipokuwa na umri wa miaka 18 na siku 145. Aprili 2009, Balotelli alifunga bao la Inter katika sare ya 1-1 dhidi ya Juventus, na alinyanyaswa kirangi na mashabiki wa Juventus mechi nzima, pamoja na nyimgo kama "hakuna Mitaliano Mweusi". Hii ilisababisha Massimo Moratti kusema kwamba iwapo angekuwa, angeiambia timu yake iwache kucheza. Nyimbo hizi za kubagua rangi pia yalishutumiwa na mwenyekiti wa Juventus, Giovanni Cobolli Gigli. Juventus walipigwa marufuku ya mechi moja nyumbani kwa sababu ya tukio hilo. Inter ilishinda taji la Serie A kwa mara ya nne mfululizo.

Zlatan Ibrahimovic na Balotelli

Katika msimu wake wa pili na timu ya kwanza ya Inter, Balotelli alikuwa na idadi ya matatizo ya nidhamu, hasa tatizo ambalo lilimshirikisha kocha wa Inter, Jose Mourinho ambaye alimfukuza kutoka kwa timu ya kwanza katika nusu ya pili ya msimu mwezi wa Januari. Kocha huyu mwenye raia wa Kireno alisema "mimi ninavyojua, kijana kama yeye hawezi kujiruhusu kufanya mazoezi kidogo kama wachezaji kama Figo, Cordoba, na Zanetti." Mapema msimu huo Mourinho alisema kuwa Balotelli anaonyesha ukosefu wa juhudi katika mazoezi.

Wasifu wa Kimataifa[hariri | hariri chanzo]

Kutokana na matatizo ya kisheria ya Balotelli, hakuweza kuzichezea timu za vijana wasiozidi umri wa miaka 15 na 17, kwani bado alikuwa anafikiriwa kuwa mhamiaji wa Ghana.

Mnamo 7 Agosti 2007, siku tano kabla ya siku yake ya kuzaliwa ya 17, Balotelli alipokea ombi lake la kwanza la kimataifa kutoka kwa kocha wa Ghana Claude Le Roy kushiriki katika mechi ya kirafiki dhidi ya Senegal katika Uwanja wa New Den katika mji mkuu wa London, Uingereza tarehe 21 Agosti 2007. Hata hivyo, aliikataa ombi hilo kwa kuonyesha tena utashi wake kuichezea timu ya Italia wakati atakuwa na umri wa miaka 18. Pia alisema utashi wake wa kuiwakilisha timu ya Italia katika kiwango cha kimataifa mara tu atakapopewa pasipoti ya Kiitaliano .

Kocha wa timu ya Italia ya vijana wasiozidi umri wa miaka 21, Pierluigi Casiraghi alionyesha nia yake ya kumtaja Balotelli katika kikosi chake punde tu atakapo pata uraia wa Kiitaliano. Mnamo 13 Agosti 2008, hatimaye Balotelli alipewa uraia wa Kiitaliano, na katika mkutano wa waandishi wa habari siku hiyo hiyo alisema ana nia kuichezea timu ya Italia ya vijana wasiozidi umri wa miaka 21. Mnamo 29 Agosti, Casiraghi hatimaye alimwita aje akajiunge na Azzurrini kwa mechi dhidi ya Ugiriki na Kroeshia. Alifunga bao lake la kwanza la kimataifa katika sare ya 1-1 dhidi ya timu ya Ugiriki ya vijana wasiozidi umri wa miaka 21, kisha akafunga mabao mawili dhidi ya Israeli katika mechi za kufuzu kushiriki katika shindano la Ulaya la vijana wasiozidi umri wa miaka 21 mwaka wa 2009.

Mnamo Februari 2009, kocha wa timu ya Italia ya vijana wasiozidi umri wa miaka 21,Pierluigi Casiraghi, alimshtukumu Balotelli kwa kukosa kusafiri na timu yake kutumia ndege hadi Trieste ambapo Casiraghi alikuwa na kikao cha mazoezi. Ilidaiwa kuwa Balotelli alilala kupindukia na ilimbidi ajiendeshee gari mwenyewe hadi Trieste ndiposa ajiunge na wachezaji wengine wa timu.

Balotelli alionyeshwa kadi nyekundu katika dakika ya 36 ya nusu ya kwanza katika mechi dhidi ya wenyeji Uswidi katika mashindano ya vijana wasiozidi umri wa miaka 21 ya Ulaya kwa kuzua vurugu dhidi ya Ponto Wernbloom. Hii ilikuwa baada yake kufunga katika dakika ya 23 na kuiweka timu yake juu 1-0.

Tuzo[hariri | hariri chanzo]

Internazionale
  • Trofeo Giacinto Facchetti-2007
  • Torneo di Viareggio-2008
  • Serie A 2007–08,2007–08,2008–09 na 2008–09
  • Supercoppa Italiana-2008

Takwimu ya Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Sahihi tangu 10 Oktoba 2008.

Klabu Msimu Serie A Ulaya Kikombe na Supercup Jumla
Matokeo Mabao Usaidizi Matokeo Mabao Usaidizi Matokeo Mabao Usaidizi Matokeo Mabao Usaidizi
Internazionale 2007-08 11 3 3 0 0 0 4 4 0 15 7 3
2008-09 22 8 1 6 1 2 3 1 0 31 10 3
2009-10 14 4 3 5 1 1 2 0 1 21 5 5
Jumla 47 15 7 11 2 3 9. 5 1 67 22 11

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]