Mang'oto

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mang`oto ni kata ya Wilaya ya Makete katika Mkoa wa Njombe, Tanzania. Msimbo wa posta ni 59502.

Kata ina vijiji sita: Mang'oto, Malembuli, Makangalawe, Usungilo, Ilindiwe, na Ibaga.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi wa kata walihesabiwa kuwa 3,918 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 3,781 [2] walioishi humo.

Katika historia ya uongozi wa kata, kabla kidogo na baada ya vijiji vya Ujamaaa kiongozi (mwenyekiti) wa kata alikuwa ndugu Lonati Mwapangile Sanga.

Wakazi wa kati hii hulima zaidi ngano, mahindi na numbu pamoja na mbogamboga: pia ni maarufu kwa kilimo cha shayiri katika vijiji vya Makangalawe na Ibaga. Wakazi hupanda pia miti kwa ajili ya kujipatia fedha

Ibwela ni sehemu ya soko katika kata ya Mang'oto. Sehemu hii ndipo wakazi wengi wanapopatikana: ni nje kidogo toka stendi ya kata. Bidhaa za kila aina hupatikana hapo.

Kata hiyo ina jumla ya shule 6 za msingi na 1 ya sekondari, pia ina zahanati 3. Wakazi huweza kutumia pia tiba za asili kama wakunga wa jadi walipo maeneo hayo.

Marejeo

  1. https://www.nbs.go.tz, uk 211
  2. "Sensa ya 2012, Njombe - Makete DC". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2004-01-02. Iliwekwa mnamo 2017-03-29. 
Kata za Wilaya ya Makete - Tanzania

Bulongwa | Ikuwo | Iniho | Ipelele | Ipepo | Isapulano | Itundu | Iwawa | Kigala | Kigulu | Kinyika | Kipagalo | Kitulo | Lupalilo | Lupila | Luwumbu | Mang'oto | Matamba | Mbalatse | Mfumbi | Mlondwe | Tandala | Ukwama


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Njombe bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mang'oto kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.