Mafarisayo : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
No edit summary
d roboti Nyongeza: ar:فريسيون
Mstari 10: Mstari 10:


[[an:Fariseu]]
[[an:Fariseu]]
[[ar:فريسيون]]
[[be:Фарысеі]]
[[be:Фарысеі]]
[[bg:Фарисеи]]
[[bg:Фарисеи]]

Pitio la 17:11, 4 Septemba 2010

Sanamu za udongo za Mafarisayo zilizotengenezwa na Giovanni d'Enrico huko Varallo (Italia).

Mafarisayo waliunda madhehebu mojawapo ya Uyahudi ambayo wakati wa Yesu Kristo iliweza kufikia 5% ya Wayahudi wote, lakini ilikuwa na athari kubwa katika jamii yao, kutokana na sifa ya kuwa wanadini hasa. Jina lenyewe lina maana ya waliojitenga (na wakosefu) ili kushika kiaminifu masharti yote ya Torati ya Musa.

Mafarisayo wanajulikana hasa kutokana na Injili ambazo zinawataja kwa kawaida kama wapinzani wa Yesu, ingawa yeye alikuwa anakubaliana nao katika mafundisho mengi ya imani tofauti na yale ya Masadukayo, madhehebu nyingine kubwa iliyokuwa na wafuasi hasa kati ya makuhani.

Mafarisayo walianza mwishoni mwa karne ya 2 K.K. na kuendelea kustawi hadi mwaka 70 B.K. , ambapo Yerusalemu iliteketezwa na Warumi. Maangamizi ya hekalu yalivunja nguvu ya Masadukayo na kuwaachia Mafarisayo uongozi wa dini yao.