Masadukayo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Masadukayo (kwa Kiebrania צדוקים sadukim) waliunda madhehebu muhimu ya dini ya Uyahudi wakati wa Yesu Kristo. Walikuwa na nguvu hasa kati ya makuhani. Ndiyo maana waliishiwa nguvu hekalu la Yerusalemu lilipoangamizwa na Warumi pamoja na mji mzima mwaka 70 B.K..

Walikubali Torati ya Musa tu, na kukataa vitabu vingine vyote vya Biblia. Kwa msingi huo, walikataa mafundisho yaliyoletwa na manabii, kama vile juu ya ufufuo wa wafu na uzima wa milele[1]. Katika hilo waligongana na Mafarisayo na Yesu ambaye, kadiri ya Injili, ndio waliohusika zaidi na kifo chake.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Masadukayo kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.