Lango:Afrika/Makala iliyochaguliwa
Makala iliyochaguliwa[hariri chanzo]
- 01 Januari 2012 : Nembo ya Uganda
- 01 Februari 2012 : Chuo Kikuu cha Cape Town
- 01 Machi 2012 : Eratosthenes
- 01 Aprili 2012 : Kampeni za Kivita katika Afrika ya Mashariki (Vita ya Kwanza ya Dunia)
- 01 Mei 2012 : Zanj
- 01 Juni 2012 : Jimbo Katoliki la Zanzibar
- 01 Julai 2012 : Assia Djebar
- 01 Agosti 2012 : Hifadhi ya Taifa ya Hell's Gate
- 01 Septemba 2012 : Ziwa Nakuru
- 01 Oktoba 2012 : Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Mashariki
- 01 Novemba 2012 : Hifadhi ya Serengeti
- 01 Desemba 2012 : Chuo Kikuu cha Addis Ababa
Makala iliyochaguliwa kwa Machi 2012[hariri chanzo]
Eratosthenes wa Kirene (Kigir. Ερατοσθένης ο Κυρηναίος, 276 KK - 194 KK) alikuwa mtaalamu wa hisabati, jiografia, historia na lugha na mkurugenzi wa maktaba ya Aleksandria katika Misri. Anakumbukwa hasa kama mtu wa kwanza aliyekadiria mzingo wa dunia. Anasemekana aliibuni neno la jiografia. Erastothenes alizaliwa mnamo mwaka 276 KK mjini Kirene wa Libya. Kirene ilikuwa moja ya miji iliyoundwa na Wagiriki wa Kale huko Afrika. Alienda Athens kwa masomo yake alipofundshwa na wanafalsafa na wataalamu mashuhuri. Mnamo mwaka 255 alihamia Aleksandria iliyokuwa mji mkuu wa Misri. Akawa mwalimu wa mwana wa mfalme na mwaka 236 KK alikuwa mkurugenzi wa tatu wa maktaba ya Aleksandria iliyokuwa kitovu cha elimu cha kimataifa kwa sababu ya mkusanyiko mkubwa wa vitabu.