Chata

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Lamprophis)
Chata
Chata kahawia (Boaedon fuliginosus)
Chata kahawia (Boaedon fuliginosus)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Reptilia (Wanyama wenye damu baridi na magamba ngozini)
Oda: Squamata (Mijusi, mijusi-nyungunyungu na nyoka)
Nusuoda: Serpentes (Nyoka)
Familia: Lamprophiidae (Nyoka walio na mnasaba na chata)
Fitzinger, 1843
Nusufamilia: Lamprophiinae (Nyoka wanaofanana na chata)
Fitzinger, 1843
Ngazi za chini

Jenasi 2, spishi 20:

Chata ni nyoka wasio na sumu wa jenasi Boaedon na Lamprophis katika familia Lamprophiidae.

Nyoka hawa ni warefu kiasi, sm 150 kwa kipeo lakini kwa wastani majike ni sm 60-100 na madume sm 40-70. Wana mkia mrefu kiasi, kichwa kwa umbo wa pembetatu na mboni za wima. Rangi yao ni kahawia, kahawianyekundu, kijivu au nyeusi. Kuna milia miwili myeupe pande mbili za kichwa na milia hii inaweza kuendelea mpaka mkia.

Chata hupumzika mchana katika vishimo au chini ya miamba, magogo au takataka. Huwinda usiku na hukamata panya hasa lakini ndege, mijusi na vyura pia. Waama, nyoka hawa ni muhimu sana kwa sababu wanasaidia watu kwa kuwaua wagugunaji wengi.

Nyoka hawa hawana sumu lakini spishi kadhaa hung'ata na kusababisha vidonda. Kwa kawaida huwa wanyama-vipenzi katika muda mfupi.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) A field guide to the Reptiles of East Africa. Academic Press, San Diego, CA, USA.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Chata kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.