Hellen Kijo Bisimba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Helen Kijo-Bisimba
Alizaliwa 10 Oktoba 1954
Nchi Bendera ya Tanzania Tanzania
Kazi yake Mwanaharati
Ndoa Emil Clemence Bisimba (kifo;1994)
Wazazi William Manase Kijo (Baba)
Janeth Kaunara Mcharo (Mama)
Watoto 4

Hellen Kijo Bisimba (alizaliwa mkoani Kilimanjaro, 10 Oktoba 1954) alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (Legal and Human Rights Center - LHRC) kuanzia 1/7/1996 hadi 30/6/2018.

Elimu yake[hariri | hariri chanzo]

Alisoma Shule ya wasichana Weruweru Kilimanjaro Sekondari ya Awali 'o' Level na kumaliza Sekondari ya juu 'A' level Korogwe High School Tanga. Ana watoto wanne.

Dkt. Helen Kijo Bisimba amesoma shahada ya uzamivu ya sheria katika chuo kikuu (daktari wa falsafa) Warwick Uingereza 2008 hadi 2011. Mnamo waka 2008 Dkt. Helen alipata tuzo akitambuliwa na ubalozi wa marekani nchini Tanzania kama ni mwanamke jasiri wa kwanza nchini Tanzania kwa kupigania haki za binadamu baada ya kusimama na kutoa tamko dhidi ya serikali juu ya mauaji yaliyofanyika visiwani Zanzibar kwa waandamanaji yaliyotokea mwaka 2001.[1] [2]

Kazi[hariri | hariri chanzo]

Amefanya kazi katika shirikia la LHRC kwa muda wa miaka 22 akiwa mkurugenzi mtendaji katika shirika hilo.

Dhamira yake ya kupigania na kuhamasisha haki za binadamu ilianza miaka ya sabini akiwa bado mwanafunzi wa sekondari kidato cha tano na sita mkoa wa Tanga, hii ni mara baada ya kugoma kuandika barua ya maelezo kwa mkuu wa shule iliyopelekea kusimamishwa masomo yake kwa muda.

Kitendo hiki kilimfanya awe mstari wa mbele kupigania haki za binadamu kwa miaka takribani arobaini sasa.

Dkt.Helen Kijo Bisimba amestaafu kazi tangu Julai 2018.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://allafrica.com/stories/201208090246.html
  2. Tanzania Standard Newspapers Ltd. "Helen-Kijo Bisimba: A strong selfless human rights activist". www.dailynews.co.tz (kwa Kiingereza). Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-04-04. Iliwekwa mnamo 2020-02-06. 
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Hellen Kijo Bisimba kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.