Gianluigi Buffon

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Gianluigi Buffon

Gianluigi Buffon (alizaliwa 28 Januari 1978) ni mchezaji wa mpira wa miguu akicheza katika nafasi ya golikipa.

Alikuwa nahodha wa timu ya taifa ya Italia hadi alipostaafu kuitumikia timu hiyo mwaka 2017.

Gianluigi Buffon ama 'Gigi' alitwaa tuzo mbalimbali za kimataifa na za ligi kuu nchini Italia. Ameshinda tuzo ya golikipa bora mara nne na tuzo ya golikipa bora wa michuano ya UEFA.

Timu alizowahi kuchezea ni pamoja na Parma ya hukohuko nchini Italia pamoja na Juventus F.C., pia Paris Saint-Germain F.C. (PSG) ya Ufaransa.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Gianluigi Buffon kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.