Dabarani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Dabarani (Aldebaran) katika kundinyota lake la jinsi Ng’ombe (zamani Tauri, lat. Taurus) kwa mtazamaji wa Afrika ya Mashariki
Ulinganifu wa ukubwa baina ya Aldebaran (Dabarani) na Jua; hata hivyo masi halisi ya Dabarani inafanana na Jua

Dabarani (ing. na lat. Aldebaran pia α Alpha Tauri, kifupi Alpha Tau, α Tau) ni nyota angavu zaidi katika kundinyota la Tauri (Taurus). Ni pia nyota angavu ya 14 kwenye anga ya usiku. Mwangaza unaoonekana unacheza kati ya mag 0.75 na 0.95.

Jina

Dabarani ilijulikana kwa mabaharia Waswahili tangu miaka mingi wakifuata njia yao baharini wakati wa usiku kwa msaada wa nyota. [1]. Walipokea jina hili kutoka kwa Waarabu wanaosema الدبران al-dabaran ambalo linamaanisha “anayefuata”[2] kwa sababu inafuata nyota za Kilimia katika mwendo wa anga. Kwa matumizi ya kimataifa Umoja wa Kimataifa wa Astronomia ulifuata desturi ya Kiarabu na kuorodhesha nyot hii kwa jina la "Aldebaran"[3].

Tabia

Dabarani - Aldebaran ina mwangaza unaoonekana wa Vmag 0.86 na mwangaza halisi ni -0.64. Hivyo no nyota angavu ya 14 kwenye anga ya usiku. Mwangaza wake unacheza kati ya 0.75 na 0.95.

Dabarani ni nyota ya karibu kiasi ikiwa umbali wake na Dunia ni miakanuru 65 -66 [4] . Masi yake ni M☉ 1.5- na nusukipenyo chake R☉ 45 (vizio vya kulinganisha na Jua letu) [5].

Ni nyota jitu jekundu katika kundi la spektra K5 III. Ilhali masi yake ni kidogo tu kubwa kuliko Jua letu kipenyo chake ni kubwa zaidi mara 45 na sababu yake ni ya kwamba jitu jekundu ni nyota iliyopanuka baada ya kuishiwa haidrojeni katika kitovu chake; katika hali hii kitovu cha nyota kinajikaza na myeyungano wa haidrojeni unahamia kwenye tabaka za nje za nyota. Hii inasababisha kupanuka kwa nyota na kuongezeka kwa mwangaza wake.

Tanbihi

  1. ling. Knappert 1993
  2. Wehr, Arabic-English, uk. 270 "dabara" turn one’s back, na Lane, Edward William, Arabic - English Lexicon III, uk. 862 "it follows الثريا and therefore is thus named" (yaani inafuata Kilimia)
  3. Naming Stars, tovuti ya Umoja wa Kimataifa wa Astronomia (Ukia), iliangaliwa Novemba 2017
  4. Gatewood, George (July 2008)
  5. Hatzes, A.; Cochran, W. (1993). wanataja parsek 20.43, taz. chini

Viungo vya Nje

Marejeo

  • Allen, Richard Hinckley: Star-Names and their Meanings; kwa G. E. Stechert New York, Leipzig, London, Paris 1899, ukurasa 59 (online kwenye archive.org)
  • Bond, Howard E.; Schaefer, Gail H.; Gilliland, Ronald L.; Holberg, Jay B.; Mason, Brian D.; Lindenblad, Irving W.; Seitz-Mcleese, Miranda; Arnett, W. David; Demarque, Pierre; Spada, Federico; Young, Patrick A.; Barstow, Martin A.; Burleigh, Matthew R.; Gudehus, Donald (2017). "The Aldebaran System and Its Astrophysical Puzzles: Hubble Space Telescope and Ground-based Astrometry". The Astrophysical Journal. 840 (2): 70, online hapa
  • Knappert, Jan: The Swahili Names of Stars, Planets and Constellations; The Indian Ocean Review September 1993 Volume 6 No. 3 September 1993, kurasa 6-7, ISSN 1031-2331
  • Gatewood, George (July 2008). "Astrometric Studies of Aldebaran, Arcturus, Vega, the Hyades, and Other Regions". The Astronomical Journal. 136 (1): 452–460. online hapa
  • Lane, Edward William : An Arabic - English Lexicon by in eight parts – 1872 (Perseus Collection Arabic Materials Digitized Text Version v1.1 of reprint Beirut – Lebanon 1968)

online hapa

  • Hatzes, A.; Cochran, W. (1993). "Long-period radial velocity variations in three K giants". The Astrophysical Journal. 413 (1): 339–348 online hapa