Nyoka-maji (Colubridae)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Crotaphopeltis)
Nyoka-maji
Nyoka-maji midomo-myeupe (Crotaphopeltis hotamboeia)
Nyoka-maji midomo-myeupe (Crotaphopeltis hotamboeia)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Reptilia (Wanyama wenye damu baridi na magamba ngozini)
Oda: Squamata (Mijusi, mijusi-nyungunyungu na nyoka)
Nusuoda: Serpentes (Nyoka)
Familia: Colubridae (Nyoka walio na mnasaba na kipiri)
Oppel, 1811
Nusufamilia: Colubrinae (Nyoka wanaofanana na kipiri)
Oppel, 1811
Jenasi: Crotaphopeltis
Fitzinger, 1843
Ngazi za chini

Spishi 6:

Nyoka-maji hawa ni nyoka wa jenasi Crotaphopeltis katika familia Colubridae. Kuna nyoka-maji katika familia Lamprophiidae pia, jenasi Grayia na Lycodonomorphus.

Nyoka hawa sio warefu sana, hadi sm 90 lakini sm 30-60 kwa kawaida. Rangi yao ni nyeusi, kijivu au kahawia lakini tumbo ni kijivunyeupe, njano au machungwa. Spishi moja ina midomo myeupe au njano.

Nyoka-maji hukiakia usiku wakiwinda vyura na pengine samaki.

Nyoka hawa wana sumu lakini chonge ni nyuma kwa utaya na sumu si hatari kwa watu. Wakitishwa spishi kadhaa hunyoosha kichwa katika pembetatu, kufungua midomo na kufyoa. Hata wanaweza kushambulia.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) A field guide to the Reptiles of East Africa. Academic Press, San Diego, CA, USA.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nyoka-maji (Colubridae) kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.