Mdudu Mkia-fyatuo
Mdudu mkia-fyatuo | ||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Mdudu mkia-fyatuo wa jenasi Isotoma
| ||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||
| ||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||
Oda 4:
|
Wadudu mkia-fyatuo ni wadudu wadogo bila mabawa wa nusungeli Collembola (ngeli kufuatana na wataalamu wengi) katika nusufaila Hexapoda walio na mkia kama springi. Kwa kawaida wadudu hawa wana urefu wa chini ya mm 6. Wale wa Entomobryomorpha na Poduromorpha wana kiwiliwili kilichorefuka, lakini wale wa Symphypleona na Neelipleona wana kiwiliwili cha mviringo. Fumbatio ina pingili sita au kasa. Ile ya kwanza inabeba kasiba dogo kwa upande wa tumbo (collophore) ambayo inafanya kazi katika kunywa maji. Mwishoni kwa fumbatio kuna kiambatisho kama mkia chenye umbo wa kiuma (furcula). Kiambatisho hiki kimekunjika chini ya tumbo zaidi ya muda na kushikilika kwa mvuto na muundo mdogo unaoitwa retinaculum. Kikifyatuliwa kinagonga didhi ya tabaka la chini na mdudu atupwa juu kwa nguvu mbali na mbuai au hatari nyingine. Wadudu hawa hula maada ya viumbehai na vijiumbe.