Bata, Equatorial Guinea

Majiranukta: 01°51′54″N 09°46′12″E / 1.86500°N 9.77000°E / 1.86500; 9.77000
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Bata

Lua error in Module:Location_map at line 522: Unable to find the specified location map definition: "Module:Location map/data/Equatorial Guinea" does not exist. Mahali pa Bata

Majiranukta: 01°51′54″N 09°46′12″E / 1.86500°N 9.77000°E / 1.86500; 9.77000
Nchi Bendera ya Guinea ya Ikweta Guinea ya Ikweta
Mkoa Litoral
Mwinuko m (16.4 ft)
Idadi ya wakazi (2012)
 - Wakazi kwa ujumla 250,770
  Jina la watu Batense (mmoja)
Batenses (wengi)
Kodi ya simu 08
Tabianchi Am

Bata ni mji wa bandari katika mkoa wa Litoral wa Guinea ya Ikweta. Ni makao makuu ya mkoa wa Litoral na pia ya kanda la Rio Muni. Kwenye mwaka 2015 inakadiriwa idadi ya watu 290,000 na hivyo ni mji mkubwa wa nchi hiyo.

Iko kwenye pwani ya Bahari ya Atlantiki ya kanda ya Río Muni ambayo ni sehemu ya kibara ya nchi. Bata ni kitovu cha usafiri na bandari, ambapo feri husafiri hadi mji mkuu Malabo na Douala nchini Kamerun, wakati ndege zinaweza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Bata.

Bandari ya Bata ni kati ya bandari zenye kina kirefu zaidi katika Afrika ya Magharibi. Hata hivyo, Bata haina beseni ya asili na gati lilijengwa ili kusaidia uhamisho wa shehena za meli. Bidhaa kuu zinazouzwa nje ni mbao na kahawa . [1] Bandari hiyo ilipanuliwa kwa sehemu na mikopo ya ushirikiano wa China, na uwezo wake ni tani milioni 6,5 na kontena za TEU 300,000 kila mwaka. [2]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Encyclopædia Britannica, Retrieved on June 18, 2008
  2. BRI and International Cooperation in Industrial Capacity: Industrial Layout Study, Xu Shaoshi Routledge, 14 June 2020