Baalbek

Baalbek (/ ˈbɑːlbɛk, ˈbeɪəlbɛk /; kwa Kiarabu: بعلبك, romanized: Baʿlabakk, Syriac-Aramaic: ܒܥܠܒܟ) ni mji uliopo mashariki mwa Mto Litani katika Bonde la Beqaa la Lebanoni takribani kilomita 67 (maili 42) kaskazini mashariki mwa Beirut[1], ni mji mkuu wa mkoa wa Baalbek-Hermel.[2] Katika nyakati za Kigiriki na Kirumi Baalbek pia alijulikana kama Heliopolis (Ἡλιούπολις, Kigiriki kwa "Sun City"). Mnamo mwaka 1998 Baalbek ilikuwa na idadi ya watu 82,608, wengi wao wakiwa Waislamu wa Shia, ikifuatiwa na Waislamu wa Sunni na Wakristo.[3]
Ndipo linapopatikana hekalu la Baalbek ambalo linajumuisha magofu mawili makubwa na makuu ya Kirumi, nayo ni Hekalu la Bacchus na Hekalu la Jupita. Mnamo mwaka 1984 iliandikwa katika orodha ya Urithi wa Dunia ya UNESCO.
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ إتحاد بلديات غربي بعلبك [West Baalbeck Municipalities Union] (in Arabic), 2013, archived from the original on 2021-07-23, retrieved 8 September 2015
- ↑ Mohafazah de Baalbek-Hermel. Localiban. Jalada kutoka ya awali juu ya 2017-02-21. Iliwekwa mnamo 2021-07-23.
- ↑ (1998) Syria – Lebanon, illustrated, Hunter Publishing, Inc., 202. ISBN 9783886181056.
![]() |
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.
|