Alexander von Humboldt

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Alexander von Humboldt alivyochorwa na Joseph Stieler 1843

Friedrich Wilhelm Heinrich Alexander Freiherr von Humboldt (14 Septemba 17696 Mei 1859) alikuwa mpelelezi na mwanasayansi kutoka Prussia katika Ujerumani.

Alexander alifanya utafiti muhimu katika jiografia na biolojia.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Humboldt alizaliwa mjini Berlin.

Baba yake Alexander Georg von Humboldt alikuwa mwanajeshi wa Prussia.

Kaka yake alikuwa waziri wa elimu wa Prussia na mtaalamu wa lugha.

Akiwa mtoto Alexander alipenda kukusanya mimea, konokono na wadudu.

Kati ya miaka 1799 na 1804 Humboldt alisafiri katika Amerika ya Kusini akiwa mwanasayansi wa kwanza kuandika juu ya safari yake katika maeneo haya. Alitambua tayari ya kwamba Amerika Kusini na Afrika ziliwahi kuwa bara moja kutokana na aina za mimea na wanyama zilizofanana pande zote mbili.

Baadaye aliongeza safari ya kutembelea Asia ya Kati na sehemu kubwa ya muda wake aliutumia kuandika taarifa ya safari hizi na kufanya tathmini ya yale aliyoyaona na kuyakuta.

Alijaribu kukusanya ujuzi wote wa sayansi wa wakati wake katika "Kosmos" iliyokuwa aina ya kamusi elezo yenye vitabu vitano.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii kuhusu mwanasayansi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Alexander von Humboldt kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.