Yusta na Rufina

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Wat. Yusta na Rufina, mchoro wa Murillo.

Yusta na Rufina (Sevilia, Hispania, 268 na 270 - Sevilia, 287) walikuwa dada na mdogo wake waliouawa kwa sababu ya imani ya Kikristo.

Kisha kukamatwa na gavana Diogeniano, waliteswa kikatili na kuachwa bila chakula gerezani; ndipo alipofariki Yusta[1]. Rufina alizidi kukiri imani yake hadi alipovunjwa shingo kwa sababu hiyo[2].

Tangu kale wanaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama watakatifu wafiadini.

Sikukuu yao inaadhimishwa kila tarehe 17 Julai[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.