Wainjili
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Simba, mfano wa Mwinjili Marko
Mtu, mfano wa Mwinjili Mathayo
Wainjili ni waandishi wa vitabu vya Injili vinavyoleta matendo na maneno ya Yesu Kristo.
Wakristo wanakubali kama Neno la Mungu vitabu vinne tu vya namna hiyo, yaani vile vilivyoandikwa wakati wa Mitume wa Yesu (karne ya 1 B.K.).
Waandishi wa vitabu hivyo wanatajwa kama Mwinjili Marko, Mwinjili Mathayo, Mwinjili Luka na Mwinjili Yohane.
Ng'ombe, mfano wa Mwinjili Luka
Tai, mfano wa Mwinjili Yohane
Ushuhuda wa kwanza kuwataja pamoja hao wanne ni ule wa Irenei wa Lyons (karne ya 2 B.K.)
Tangu zamani hao wanne walihusianishwa na viumbe wanne waliotajwa katika Kitabu cha Ezekieli, halafu katika Kitabu cha Ufunuo: simba, ng'ombe, mtu, tai.