Zineddine Belaïd

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Zineddine Belaïd, ( alizaliwa 20 Machi, 1999) ni mwanasoka wa Algeria ambaye anacheza kama beki wa kati klabu ya USM Alger katika Ligi ya Algeria Professionnelle 1 na timu ya taifa ya Algeria A'.[1][2][3]

Kazi[hariri | hariri chanzo]

Mnamo Mei 31, 2018, Zinedine Belaid alisaini mkataba wake wa kwanza wa kikazi na klabu ya NA Hussein Dey na kucheza mechi yake ya kwanza katika kiwango cha kulipwa mnamo Januari 20, 2019 kwenye Kombe la Shirikisho la CAF dhidi ya klabu ya Al-Ahly Benghazi ya Libya, katika msimu wake wa kwanza pekee alicheza mechi tatu.

Ushiriki Kimataifa[hariri | hariri chanzo]

Mnamo Juni 2021, Zineddine Belaïd aliitwa na Kocha Madjid Bougherra kwa mara ya kwanza kwenye timu ya taifa ya Algeria A' dhidi ya Liberia ili kuzindua uwanja mpya wa Oran kwa ushindi wa 5-1.

Heshima[hariri | hariri chanzo]

USM Alger

  • Kombe la Shirikisho la CAF: 2022–23

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "FICHE DU JOUEUR: ZINEDDINE BELAID". 
  2. "Zineddine Belaïd". 
  3. "Zineddine Belaid à l’USM Alger". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-10-23. Iliwekwa mnamo 2023-06-12. 

Viungo Vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Zineddine Belaïd kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.