Wanaisraeli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kwa maana mbalimbali ya jina Israeli tazama Israeli (maana)


Wanaisraeli ni namna ya kutaja watu wa Agano la Kale waliokuwa wazawa wa Yakobo aliyeitwa pia Israeli, mmoja wa mababu wa taifa la Israeli ya Kale pamoja na babu yake Abrahamu na baba yake Isaka.

Kadiri ya kitabu cha Mwanzo Yakobo alipewa na Mungu jina la "Israeli" baada ya kushindana naye kwenye mto Yaboki.

Alizaa wana wa kiume 12 waliokuwa mababu wa makabila 12 ya Israeli ya Kale.

Katika maandiko ya Biblia ya Kiebrania (Tanakh) na kwa hiyo pia katika Agano la Kale la Biblia ya Kikristo makabila haya mara nyingi huitwa "Waisraeli", "wana wa Israeli" au pia "watu wa Israeli".

Kwa historia yao angalia Israeli ya Kale.